Quantcast
Channel: BONGOWEEKEND
Viewing all 1934 articles
Browse latest View live

TBL YQZINDUA KAMPENI YA 'CASTLE LITE UNLOCKS' JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL),  Idara ya Kuunganisha Wateja Afrika Mashariki, George Kavishe (kulia), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, wakati wa uzinduzi wa kampeni ijulikanayo, ‘Castle Lite Unlocks’. Kushoto ni Meneja Chapa Msaidizi wa Bia Laini Tanzania, Isaria Kilewo na katikati ni Meneja Masoko wa TBL Kitengo cha Bia Laini Afrika Mashariki, Amou Majok.


 Meneja Masoko wa TBL Kitengo cha Bia Laini Afrika Mashariki, Amou Majok (katikati), akizungumza kwenye mkutano huo.
 Mkutano ukiendelea.
 Waandishi wa habari wakiwa katika uzinduzi huo.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
 Wadau wakibadilishana mawazo katika mkutano huo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.


Na Dotto Mwaibale

KAMPUNI ya kutengeneza Bia  Tanzania (TBL)) leo imezindua kampeni ijulikanayo, ‘Castle Lite Unlocks’ ambayo lengo lake ni kuhamasisha wateja wake wa bia chapa Castle Lite kuifurahia zaidi na pia kuwaleta pamoja katika tamasha kubwa litalofanyika mwezi wa Julai mwaka huu.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa hafla ya uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika katika ofisi za TBL zilizoko Masaki, Meneja Masoko wa TBL Idara ya Kuunganisha Wateja Afrika Mashariki, George Kavishe, alisema TBL kwa miaka imekuwa ikijikita katika kuwafurahisha na kuwachangamsha wateja wake, hasa vijana kwa matamasha ikiwemo muziki ambao upo katika vipaumbele vya kampuni hiyo.   

“Uzinduzi huu utafikia kilele chake tarehe 22 mwezi wa Julai mwaka huu ambapo kutakuwa na tamasha kubwa Dar es Salaam litakalowapa nafasi wateja wetu kushuhudia wanamuziki wakubwa wa ndani na nje ya nchi, hivyo kuwapa wateja burudani itakayokuwa kwenye kumbukumbu zao kwa muda mrefu”, alisema Kavishe.   

Kavishe aliongeza kuwa kwa kipindi hicho cha miezi mitatu ya kampeni, zawadi kedekede zitatolewa zikiwemo muda wa maongezi wa simu za mkononi wa zaidi ya milioni 30 na pia tiketi zaidi ya elfu moja kwa washindi wa droo ambazo zitakuwa zinashindanishwa.

Aliongeza kwamba bajeti ya kampeni nzima ni zaidi ya shilingi milioni mia saba.

Naye Meneja Masoko wa TBL Kitengo cha Bia Laini Afrika Mashariki, Amou Majok alisema kuwa TBL ina utaratibu mahsusi wa kuandaa matamasha mara kwa mara ili kuwashukuru wateja wake kwa kuwapa burudani na kuwahamasisha kuzifurahia vinywaji vyake ambavyo ni vya hali ya juu na vyenye ubora zaidi.   


HIVI NDIVYO INTERNETI INAVYO ATHIRI MAISHA YAKO YA KILA SIKU

$
0
0


Na Jumia Travel Tanzania

Hakuna kitu kinachoudhi kama kuwa sehemu na marafiki, familia au ndugu lakini unakuta kila mtu ameinamia skirini ya simu yake! Kwa kiasi kikubwa kuja kwa mtandao wa intaneti kumewafanya watu kujikita zaidi na simu zao badala ya watu au kufaidi mazingira yanayowazunguka.

Kuna tafiti nyingi zimekwishafanyika na kuthibitisha kuwa muda mwingi unaotumika kwenye intaneti una madhara kama vile ya kimwili na kiakili. Mbali na kuwepo kwa faida lukuki za mtandao huo, Jumia Travel ingependa kukujulisha kuwa yafuatayo yanaweza kukumba endapo utautumia vibaya: 
Intaneti husababisha hali ya kujisikia vibaya, kukosa furaha na wivu. Mtu anaweza kushangaa na kujiuliza hii inaweza kutokeaje. Jibu ni rahisi sana. Mambo tunayoyaona kwenye mitandao ya kijamii yanayowekwa na watu maarufu, ndugu, jamaa au marafiki wa karibu huweza kukukosesha furaha kwa namna moja ama nyingine. Hebu jaribu kufikiria unamuona rafiki yako wa karibu ameweka picha zake akiwa amesafiri sehemu ambayo wewe hujawahi kufika au chakula usichowahi kukila utajisikiaje? Ingawa sio wote wanaoweza kujisikia vibaya lakini kwa asilimia kubwa wengi wao hupatwa na wivu au kusononeka nafsi kuona kwamba inawezakana wao wasije kuwa na maisha kama yale. 
Intaneti husababisha watu wengi kujihisi kuwa wanapitwa na wakati. Tangu enzi za kale kila nyakati zimekuwa na mitindo tofauti ya maisha hapa duniani. Kwa bahati mbaya sio watu wote ambao wanao uwezo wa kuendana na mitindo au fasheni zilizopo. Hali hii imewafanya wengi kujihisi kupitwa na wakati endapo wasipoishi kama wanavyoona kwenye mitandao. Kupitia mitandao ya kijamii kama vile Instagram watu wanaweza kuwashirikisha wenzao picha na video za namna wanavyoishi kuendana na wakati. Ambapo mara nyingi yale yanakuwa sio uhalisia wa maisha yao.    

Intaneti imekuwa ni chanzo kikubwa kwa watu wengi kutokuwa na utulivu wa akili. Nadhani hii hali inawakuta watu wengi katika maisha yao ya kila siku katika ulimwengu wa sasa wa intaneti. Kuna wakati unajaribu kujikita kwenye suala fulani lakini shughuli zinazoendelea mtandaoni kupitia simu yako ni kikwazo kikubwa. Kwa mfano, unataka kukamilisha kazi uliyopewa na bosi wako, mara ujumbe wa Whatsapp umeingia, hujatulia Facebook, Twitter na Instagram nazo zote zinakujulisha kuwa unapitwa huku. Kwa hali hii sidhani kama kuna jambo ambalo mtu anaweza kulikamilisha kwa ufanisi na usahihi unaohitajika.
Intaneti inawanyima watu fursa ya kufurahia maisha halisi yanayowazunguka. Kwa sasa ni jambo la kawaida kabisa sasa kuona familia imekwenda hotelini kupata chakula pamoja na kubadilisha mazingira ya nyumbani lakini ukakuta kuanzia watoto mpaka wazazi wote wameinamisha nyuso zao kwenye skirini za simu zao. Hakuna tena ile hali ya zamani kwamba muda wa chakula ndipo familia hukutana kwa pamoja, kuzungumza, kucheka na kubadilishana mawazo juu ya yale waliyoyapitia siku nzima. Kwa hali ilivyo sasa hivi huwezi kusikia tena vicheko au gumzo kwenye familia nyingi kwani vyote hivyo vimeamia kwenye simu. Usishangae ukamuona mtu anacheka mwenyewe ukadhahania ni punguani, hapana, ni mambo ya intaneti hayo.

Intaneti imekuwa ni chanzo kikubwa cha watu kutokuwa wabunifu katika masuala mbalimbali. Hebu jaribu kufikiria ingekuwaje kama hizo video unazozitazama kupitia YouTube, habari unazoziona Facebook au Twitter, au picha unazoziona kupitia Instagram; vyote hivyo ungevipataje kama waliogundua nao wangekuwa wanatumia muda wao kwenye intaneti kupitia kazi za wenzao. Hii inamaanisha kwamba hatupaswi kutumia muda mwingi kuwa watumiaji wa vitu vya kwenye intaneti badala yake nasi tuwe wazalishaji ili kuwanufaisha na wengine zaidi. Unaweza kukuta mtu tangu siku inaanza mpaka inaisha yeye anaimaliza kwenye mitandao ya kijamii akipitia, kutazama na kusoma habari za watu wengine.
Yaliyozungumzwa katika makala haya ndio maisha ya wengi kwa sasa jinsi yalivyoathiriwa na kuja kwa intaneti. Lakini zipo mbinu kadhaa za kuweza kujiepusha na madhila hayo yote. Jumia Travel inashauri kwamba jukumu la mtu kuepukana na uraibu wa matumizi ya intaneti ni la kwake mwenyewe. Kwa mfano, kujiwekea au kutenga muda maalumu wa kuingia mtandaoni, kuzima ishara zitokanazo na mitandao ya kijamii au kuzima kabisa intaneti kwenye simu yako mpaka muda fulani inaweza kusaidia pia.   

TAMKO LA WAZIRI UMMY MWALIMU KATIKA KUADHIMISHA SIKU YA MALARIA DUNIANI

KILA MTANZANIA AHAKIKISHE ANALINDA MUUNGANO

$
0
0

Na. Immaculate Makilika, MAELEZO -DODOMA ​

Kila mtanzania ametakiwa kuhakikisha anafanya jitihada za kuimarisha na kulinda Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulioasisiwa miaka 53 iliyopita.

Akizungumza leo wakati akihutubia wananchi katika sherehe za Maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano katika uwanja wa Jamhuri uliopo mjini Dodoma, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alisema kuwa ni muhimu watanzania wakalinda Muungano kwa vile una manufaa kwa nchi zote mbili.

“Kila mtanzania ahakikishe anafanya jitihada za kuimarisha na kulinda Muungano wetu, kwa vile Muungano na amani iliyopo nchini ndio chachu ya maendeleo yetu” alisema Rais Magufuli. Rais Magufuli alisisitiza kuwa “Muungano ndio silaha yetu, ni nguvu yetu, mimi na mwenzangu Dkt. Shein tutaulinda Muungano kwa nguvu zote na yeyote atakayejaribu kuuvunja atavunjika yeye” alisema Rais Magufuli.

Akitaja baadhi ya mafanikio yaliyopatikana katika miaka 53 ya Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar ni pamoja na kuunganisha mataifa mawili na kuunda taifa moja lenye nguvu. Rais Magufuli alisema mafanikio mengine ni pamoja na kuwa ni kuimarisha miundombinu ya usafiri wa anga, majini, nchi kavu na reli, kukabiliana na matatizo ya umaskini, ukosefu wa ajira na kukua kwa uhusiano wa diplomasia kati ya Tanzania na mataifa mbalimbali ambapo yamepelekea mafanikio katika nyanja za kiuchumi, kisiasa, na jamii.

Aidha, hii ni mara ya kwanza kwa sherehe za Maadhimisho ya Muungano kufanyika mkoani Dodoma ambapo, Rais Magufuli alisema kuwa Serikali imeendelea kufanya jitihada mbalimbali za kujenga miundombinu ili kufikia azma yake ya kuhamishia makao yake makuu mjini Dodoma ifikapo mwaka 2020.

“Niwahakikishie wana Dodoma na Watanzania kwa ujumla kwamba Serikali sasa tumefika Dodoma na hatutarudi nyuma tena,ambapo awamu ya kwanza ya watumishi wa Serikali takribani 3,000 kwa ngazi za Mawaziri,Naibu Waziri,Makatibu wakuu na Manaibu Katibu wakuu wameshahamia Dodoma, kama tulivyoahidi kufikia mwaka 2020, Serikali yote itakuwa imehamia hapa”, alisisitiza Rais Magufuli.

Sherehe za Maadhimisho ya miaka 53 ya Muungano zenye kauli mbiu isemayo “Miaka 53 ya Muungano, tuulinde na kuimarisha, tupige vita dawa za kulevya na kufanyakazi kwa bidii”, zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wajane wa viongozi waasisi wa Muungano ambapo ni Mama Maria Nyerere na Mama Shadya Karume.

IVORY YAPANIA KUPAA ANGA ZA MUZIKI WA DANSI

$
0
0
Ijumaa hii na kila Ijumaa ni siku ya raha na starehe kwa wakazi wa Tabata na vitongoji vyake, maana mara tu baada ya jua kuzama kiota maarufu cha Next  Door kilichopo katika kitongoji hicho cha wastaarabu huwaka moto wa midundo ya aina mbalimbali inayoporomoshwa na Ivory  Band iliyosheheni vipaji visivyo vya kawaida. 

Ripota wa Globu ya Jamii alipotembelea hapo katika ukumbi wa Next Door Ijumaa hakuweza kuamini macho na masikio yake kukuta ukumbi umefurika mashabiki wakipata burudani toka kwa vijana hao. Akaamua kuhoji wahusika. 

“Bendi hii tulianzisha mwaka jana (2016) mwezi wa tano na wamiliki wake ni sisi wanamuziki wenyewe tukishirikiama na wenzetu kadhaa ambao tumewaajiri”, alisema mmoja wa wamiliki wa Ivory Band , Rama Pentagone, wakati wa mapumziko mafupi. 
Pentagone, anayepiga kinanda, gitaa na kuimba alisema wamiliki wa bendi hiyo ni yeye, mwanamuziki mkongwe mwenye sauti tamu Saleh Kupaza, Omari Kisila na Amina Juma. 'Ibory Band' bado hatujatoa mtindo wa kutumia kwa sababu sisi tunapiga muziki tofauti na wengie wengine, hasa ukizingatia kwamba hatupigi “Sebene”, alisema Pentagone. 

Saleh Kupaza aliyekuwa pembeni akipoza koo na maji alisema hatua ya kwanza ya kuanzisha bendi na kujiajiri wao wenyewe imefanikiwa kwa asilimia 100, na kwamba sasa wako katika hatua ya pili ambayo ni kuazalisha nyimbo kibao zenye mtazamo wa kitaiafa na kimataifa. 

“Malengo yetu ya mbeleni ni kuwa kundi la muziki la Kimataifa na endapo Mungu atatujalia kutimiza malengo yetu ni kufanya maonesho makubwa ndani na nje ya nchi”, alisema Kupaza. 


Omari Kisila akaongezea kwamba kwa kuwa inakaribia watimize mwaka mmoja toka waanze rasmi, IVORY BAND imepanga kufanya bonge la onesho litakaloandamana na sherehe za bendi hiyo kutimiza mwaka mmoja mnamo mwezi wa Julai. 

“Tumeamua kufanya onesho hilo kabambe mwezi wa Saba kwa sababu mwezi Mei na Juni utakuwa ni Mwezi Mtukufu wa Ramadhani unaotarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Mei na kumalizikia mwezi Juni”, alisema Kisila. 
Amesema ukumbi pamoja na tarehe rasmi ya kufanyika tukio hilo vitatangazwa muda utapokaribia, na kwamba kwa sasa wako katika hatua za mwisho za kuanza kupasua anga za redio na TV kwa kutoa kibao chao cha utambulisho kiitwacho SHIKA MOYO unachokisikia hapo chini. Hicho ni moja ya vibao takriban kumi ambavyo husisimua mashabiki kila wapigapo.
  

SSRA YASHIRIKI MAONESHO YAUSALAMA MAHALI PA KAZI MKOANI K'NJARO

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Kazi, na Watu wenye Ulemavu, Mh. Jenista Mhagama, akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Meneja wa Rasilimali watu na Utawala wa Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) Bi Amina Ally aliotembelea banda la SSRA wakati wa Maonyesho ya Maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa kazi (OSHA) yanayoendelea mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Kazi na Watu wenye Ulemavu, Mh. Jenista Mhagama akiatoa maelekezo wakati alipotembelea banda la Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) kwenye Maonyesho ya Maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa kazi (OSHA) yanayoendelea mjini Moshi mkoani Kilimanjaro. 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Kazi na Watu wenye Ulemavu, Mh. Jenista Mhagama, akimkabidhi cheti cha Ushiriki Kaimu Meneja wa Rasilimali watu na Utawala wa Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA). Bi. Amina Ally wakati wa kilele cha maonesho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi yanayoendelea Mjini Moshi, mkoani, Kilimanjaro.   
Afisa Matekelezo wa Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), akigawa vipeperushi kwa wananchi waliotembelea banda la SSRA wakati wa Maonesho ya OSHA yanayondelea Mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro. 
Afisa Uhusiano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bw. Ally Masaninga akitoa maelezo kwa wananchi waliotembelea banda la SSRA, wakati wa Maonesho ya OSHA yanayondelea Mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro. 
Maafisa wa SSRA, wakitoa ufafanuzi juu ya Masuala yanayohusu Sekta ya Hifadhi ya Jamii kwa wadau waliotembelea banda la mamlaka hiyo, wakati wa Maonesho ya OSHA, yanayoendelea Mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro.
Wananchi wakisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa wa SSRA, wakati wa maonesho ya OSHA, yanayofanyika mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro. 
Wadau waliotembelea banda la SSRA, wakijipatia vipeperushi wakati wa maonesho ya Maadhmisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi yanayofanyika Mkoani Kilimanjaro.

MKUU WA MKOA WA PWANIMHANDISI NDIKIRO AISHUKURU TANESCO KWA MSAADA WA USAFI

$
0
0
 Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikiri, (kulia), akipeana mikono na Kaimu Meenja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), Leila Muhaji, wakati akipokea msada wa vifaa vya kufanyia usafi kwa ajili ya kituo cha Afya Mkoani mjini Kibaha Aprili 29, 2017.
 NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
MKUU wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikiro, ameishukuru TANESCO kwa msaada wake wa vifaa vya kufanyia usafi kwa ajili ya Kituo cha Afya Mkoani Mjini Kibaha.


Mhandisi Ndikiro alisema, hatua hiyo yaTANESCO ni ushahidi tosha wa kuunga mkono jitihada za serikali za kuhakikisha wananchi wanapatiwa huduma afya katika mazingira ya usafi.
"Niseme tu mlichokifanya ni kitu kizuri sana, na ningeshauri taasisi nyingine za umma na binafsi, kutoa sehemu ya faida wanayopata kutokana na shughuli zao na kurudisha kwa umma kwa njia ya kusaidia shughuli za kijamii kama hii ya usafi." alisema.

Naye Kaimu Meneja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), Bi Leila Muhaji alisema, TANESCO  kama mtoa huduma ya umeme kwa Wananchi na ikitambua kuwa wananchi ndio wateja wake wakubwa, pia imeona ni busara kusaidia serikali katika kuhakikisha mazingira yanayowazunguka kama vile kituo hiki cha afya yanakuwa safi." alisema.

Bi. Leila pia alisema, TANESCO imetoa vifaa hivyo ili kuunga mkono juhudi za serikali za kuhamasisha umma kufanya usafi wa jumla kila mwisho wa wiki. "Tumeungana nanyi leo Jumamosi ambayo ni siku ya usafi, ili tufanye usafi pamoja kwenye kituo chetu hiki cha afya, kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, napenda muwashukuru sana na mpokee msada wetu huu mdogo ambao nina hakika utasaidia kwa sehemu fulani katika kuweka mazingira ya hospitali yawe safi." alsiema

Awali Mkuu wa Mkoa Mhandisi Ndikiro, aliwaongoza watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha, wafanyakazi wa TANESCO Mkoa wa Pwani na wachache kutoka makao makuu katika zoezi la kufanya usafi wa mazingira kwa kufyeka nyasi kuzunguka mazingira ya kituo hicho cha afya.
 Mhandisi Ndikiro, akiwa na Mganga Mkuu wa Mji wa Kibaha, akitoa hotuba yake
 Bi leila Muhaji, (katikati), akitoa hotuba yake, Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikiro, na Meneja Rasilimali watu TANESCO mkoa wa Pwani, Bi.Nisile Mwakalinga
 Wafanyakazi wa TANESCO Mkoa wa Pwani
 Mhandisi Ndikiro akimshukuru Bi.Nisile, huku Bi. Leila (wapili kushoto) na Bi Salama Juma, ambaye ni Afisa Uhusiano TANESCO
 Wafanyakazi hawa wa TANESCO wakiwa wamebeba sehemu ya vifaa hivyo
 Mhandisi Ndikiro, (kulia) na Bi. Leila Muhaji wakifyeka majani kwenye eneo la Kituo hicho cha Afya
Wafanyakazi wa TANESCO wakifagia mazingira kuzunguka kituo hicho
 Mganga Mkuu wa Mji wa Kibaha, akifafanua baadhio ya mambo kwa waandishi wa habari
 Watumishi wa Halmashauri ya mji wa Kibaha, wakifyeka nyasi
 Baadhi ya wafanyakazi wa TANESCO
 Baadhi ya wafanyakazi wa TANESCO
 Mhandisi Ndikiro akiwa amenyanyua baadhi ya vifaa alivyokabidhiwa
 Watumishi wa kituo hicho cha afya wakikusanya sehemu ya vifaa hivyo
Mtumishi wa kituo cha Afya cha Mkoani mjini Kibaha, akwia amebeba sehemu ya vifaa hivy

DKT. MWANYEMBE AHWATAKA VIJANA KUTENGA MUDA WA KUJISOMEA

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mkwakyembe (kulia) akiwa amepokelewa na Mwandishi wa kitabu cha'Colour of Life' Ritha Tarimo siku ya uzinduzi wa kitabu hicho leo 30 Aprili, 2017 Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mkwakyembe pamoja na wageni waalikwa wakiangalia video inayoelezea maduhui ya kitabu cha "Colour of Life" kilichoandikwa na Mwandishi wa vitabu Bi. Ritha Tarimo, 30 Aprili, 2017 Jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mkwakyembe akiongea na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa kitabu cha "Colour of Life" kilichoandikwa na Mwandishi wa vitabu Bi. Ritha Tarimo 30 Aprili, 2017 Jijini Dar es Salaam.


Mwandishi wa vitabu Ritha Tarimo akiongea na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa kitabu chake cha 'Colour of Life'.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mkwakyembe akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kitabu cha "Colour of Life" kilichoandikwa na Mwandishi wa vitabu Ritha Tarimo. 30 Aprili, 2017 Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mkwakyembe akiwa katika picha ya pamoja na familia ya Mwandishi wa vitabu +Ritha Tarimo mara baada ya uzinduzi wa kitabu hicho 30 Aprili, 2017 Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mkwakyembe akiwa katika picha ya pamoja na familia ya Mwandishi wa vitabu Ritha Tarimo pamja na wageni waalikwa mara baada ya uzinduzi wa kitabu hicho 30 Aprili, 2017 Jijini Dar es Salaam.
(PICHA/HABARI NA BENEDICT LIWENGA-WHUSM)


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amewataka vijana kutumia muda wao kujenga utamaduni wa kujisomea vitabu badala ya kupoteza muda wao mwingi katika mitandao ya kijamii kwakuwa kusoma vitabu ndiyo msingi mzuri wa elimu.


Kauli hiyo ameitoa leo Jijini Dar es Salaam wakati alipokuwa akizindua Kitabu cha “Colour of Life” kilichoandikwa na Mwandishi  Ritha Tarimo  ambapo katika hotuba yake aliyoitoa mbele ya wageni waalikwa amesisitiza suala la vijana kujenga utamaduni wa kupenda kusoma vitabu ili kukuza elimu yao.


Mhe. Mwakyembe ameeleza kuwa, baadhi ya vijana siku hizi wamekuwa wakitumia muda wao mwingi katika mitandao ya kijamii badala ya kujisomea, hivyo amewashauri wajifunze kutoka kwa Mwandishi wa Kitabu hicho ili waje kuwa waandishi hodari wa kutegemewa na Taifa.


Sambamba na rai hiyo, Waziri Mwakyembe amempongeza Ritha Tarimo kwa juhudi zake kubwa na maarifa katika kutunga na kuandika kitabu hicho ambacho amesema kuwa kitabu hicho ni kizuri na kina maudhui mazuri kwa vijana hususani wanafunzi, hivyo ameitaka jamii kumuunga mkono kwa kukisoma ili jamii ipate kuelimika.


“Ukimkuta mtu kama Ritha Tarimo anaandika kitabu katika kipindi hiki ambapo vitabu vinaonekana kuondolewa kwasababu ya maendeleo ya teknolojia, ni vema kumpa moyo na kumuunga mkono kwakuwa yeye ametuonyesha Watanzania kuwa hata sisi tunaweza, na kitabu hiki niwaambie ukweli kina maudhui ya kumtia moyo kijana ya kutokata tamaa katika maisha”, alisema Dkt. Mwakyembe.


Ameongeza kuwa, Serikali inauunga mkono juhudi zake za uandishi wa vitabu vyake na amechukua baadhi ya nakala za kitabu hicho kwa ajili ya kuzipelekeka kwa Waziri husika wa masuala ya Elimu Sayansi na Teknolojia ili kuona namna gani kitabu hicho kinaweza kuisaidia jamii.


Kwa upande wake Mwandishi Ritha Tarimo ameishukuru Serikali kwa kukubali wito wa kukizindua kitabu chake na pia utayari wa Serikali katika kumuunga mkono ili uandishi wake uwe wenye tija kwa jamii ya Watanzania.


Ameeleza kwamba, kazi ya uandishi ameinza muda mrefu na leo ameweza kupata nafasi ya kuungwa mkono na Serikali pamoja na Watanzania mbalimbali ikiwemo familia yake na hatimaye kukamilisha kitabu hicho na kukizindua rasmi.


“Nakushukuru Mhe. Waziri kwa kutumia muda wako kuja kukizindua kitabu hiki, nakushukuru sana na sasa naamini ndoto zangu zinatimia, kitabu hiki nimekitengeneza katika umbo dogo ili kiweze kuwavutia watu wengi kwani kina maudhui mazuri kwa vijana na jamii nzima ya Kitanzania”, alisema Ritha.


Kitabu cha Colour of Life ni moja kati ya vitabu saba alivyoandika Mwandishi huyo ambacho pia kimepata fursa ya kuzinduliwa na Waziri Dkt. Harrison Mwakyembe na kwa mujibu wa mwandishi huyo, kitabu hicho kina maudhui mazuri kwa vijana katika kuwajenga kimaisha.

NEC YATANGAZA NAFASI YA WAZI KITI CHA MBUNGE WA VITI MAALUM CHADEMA DR. ELLY MARKO

$
0
0



Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza kuwepo kwa nafasi wazi ya Mbunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo – CHADEMA,  kufuatia kifo cha Mbunge wa Viti Maalum wa chama hicho Mhe. Dr. Elly Marko Macha aliyefariki tarehe 31 Machi 2017.

Akitoa taarifa ya nafasi hiyo kuwa wazi Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji wa Rufaa Mhe. Semistocles Kaijage amesema kuwa kwa mujibu wa Kifungu cha 37 (3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343, Mhe. Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameijulisha Tume juu ya kuwepo kwa nafasi wazi ya Mbunge huyo.

Amesema taratibu za kujaza nafasi hiyo zinaendelea kwa kuzingatia Ibara ya 78 (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ikisomwa pamoja na kifungu cha 86A (8) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343.

TAASISI YA KILIMANJARO DIALOGUE WAADHIMISHA SIKU YA UHURU WA HABARI DUNIANI

$
0
0
 Mdhamini wa Taasisi ya Kilimanjaro Dialogue, Habib Miradji (katikati) akiongoza mjadala jijini Dar es Salaam leo, kuhusu umuhimu wa wanahabari kuandika habari za kudumisha amani nchini ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani. Mjadala huo uliandaliwa na taasisi hiyo.
 
      (PIVHA NA RICHARD MWAIKENDA)
  Mdhamini wa Taasisi ya Kilimanjaro Dialogue, Habib Miradji (katikati) akiongoza mjadala jijini Dar es Salaam leo, kuhusu umuhimu wa wanahabari kuandika habari za kudumisha amani nchini ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Habari Duniani. Mjadala huo uliandaliwa na taasisi hiyo. Kutoka kulia ni Rais wa taasisi hiyo, Ali Akkiz na Mshauri wa masuala ya Habari, Felix Kaiza.
 Mshauri wa Masula ya Habari, Felix Kaiza akielezea umuhimu wa wamiliki wa vyombo vya habari kuweka utaratibu wa mafunzo ya ndani (In House Training) kwa waandishi wa habari ili kuinua weledi pia alishauri kuwepo na Exchange Program kati ya vyombo vya habari nchini na nje ya nchini jambo ambalo huwaongezea uwezo wanahabari.
 Mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha Chanel Ten, Esther Zaramula akielezea kwenye mjadala huo jinsi alivyonufaika na mpango wa kubadilishana uzoefu
 Habib Miradji akisisitiza jambo wakati wa mjadala huo ambapo alifafanua zaidi umuhimu wa wanahabari kuandika habari kwa kufuata maadili na kusimamia kwenye ukweli.

Pia katika kongamano hilo waliwaasa wanahabari kutojiingiza katika mkumbo wa kuingizwa mifukoni mwa wanasiasa na matajiri kwa kuandika habari za kuwasifia wao badala ya maslahi ya wananchi.
 Mwandishi wa habari, Ezekiel Kamwaga  akielezea umuhimu wa wanahabari kujiendeleza kielimu pamoja na vyombo vya habari kubadilika kwa kwendana na kasi ya mabadiliko ya kizazi hiki cha maendeleo ya teknolojia ya habari.
Rais wa taasisi ya Kilimanjaro Dialogue, Ali Akkiz aktoa shukrani kwa wanahabari walioshiriki kwenye mjadala huo uliofanikiwa.

UFAFANUZI KUHUSJ UTAFITI WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA IKIMWI

$
0
0


Kumekuwepo na taarifa iliyoandikwa kwenye kurasa za mitandao ya kijamii za Clouds Media Group za Facebook na Instagram ikimnukuu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Dkt. Grace Magembe akisema kuwa ‘‘Upimaji wa VVU nyumba kwa nyumba sasa rasmi, mchakato unaendelea na zoezi litaanza rasmi mwishoni mwa mwezi huu“.

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kwa mara nyingine, inapenda kutoa ufafanuzi kwamba UKIMWI haupimwi  nyumba  kwa nyumba  bali inafanya utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania ambapo UKIMWI ni ugonjwa mmojawapo unaopimwa katika utafiti huu.

Aidha, utafiti huu unafanyika kwenye kaya chache ambazo zimechaguliwa kitaalam nchi nzima ili ziweze kuwakilisha kaya nyingine ambazo hazihusiki moja kwa moja.

Utafiti huu unajumuisha kaya zipatazo 16,000 ambazo ni sampuli iliyochaguliwa kisayansi kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar na unahusisha watu wazima wasiopungua 40,000 na watoto takribani 8,000. Kwa Dar es Salaam, utafiti huu wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI utahusisha kaya zisizozidi 1,000 kati ya kaya 1,000,000 na unatarajia kuanza tarehe 31 Mei, 2017 na kuendelea kwa wiki zisizozidi tatu (3).

Mbali na upimaji wa UKIMWI, utafiti huu pia unapima kiwango cha maambukizi ya Kaswende, Homa ya ini (Hepatitis B), uwepo wa viashiria vya usugu wa dawa, maambukizi mapya ya VVU, kiwango cha VVU mwilini kwa watu wanaoishi na VVU (Viral load), wastani wa maambukizi ya VVU kwa watu wa rika zote pamoja na wingi wa chembechembe za kinga mwilini (CD4 T-cell count). Aidha, kupima ni hiari na watakaogundulika kuwa na maambukizi, watapata rufaa ya kwenda kupatiwa matibabu bure katika vituo vya kutolea huduma za afya. Ifahamike kwamba, utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI wa mwaka 2016/17 unafanyika nchini kwa mara ya nne (4) ambapo utafiti wa kwanza ulifanyika mwaka 2003, wa pili mwaka 2007 na wa tatu mwaka 2011.

Hivyo, NBS inapenda kuwatoa hofu Wananchi kuwa, kufanyika kwa utafiti huu sio jambo jipya na Watanzania ambao wamekuwa wakipitiwa na utafiti huu, wamekuwa wakitoa ushirikiano kwa zaidi ya asilimia 90 na mpaka sasa utafiti huu umeshafanyika katika mikoa 17 ya Tanzania Bara na kwa upande wa Tanzania Zanzibar, utafiti huu umekamilika katika maeneo yote yaliyochaguliwa.

Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania unaendelea kufanyika nchini, ukisimamiwa na NBS kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Tanzania Bara, Wizara ya Afya kwa Tanzania Zanzibar, Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar (OCGS), Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) na Tume ya UKIMWI Zanzibar (ZAC). Imetolewa na: Mkurugenzi Mkuu, Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).

WAANDISHI WATAKIWA KUTUMIA KALAMU ZAO VIZURI

$
0
0

Na Nuru Juma & Husna Saidi- MAELEZO

Waandishi wa Habari nchini wametakiwa kuzingatia kanuni,sheria na taratibu za uandishi katika kuandika habari zitakazoleta umoja,mshikamano na maendeleo na siyo uchochezi ili kujenga jamii bora.

Hayo yamesemwa leo Jijini Mwanza na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt.Harrison George Mwakyembe kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani. Dkt. Mwakyembe aliongeza kwa kusema kuwa Serikali inatambua umuhimu wa siku ya uhuru wa vyombo vya habari ambapo siku hiyo huwa maalum kwa wadau wa tasnia hiyo kukutana na kujadiliana mambo mbalimbali ikiwa ni njia ya kujenga jukwaa la ushirikiano.

“Uhuru wa habari una ukomo wake hivyo ni muhimu kwa vyombo vya habari hapa nchini kuajiri watu wenye taaluma hiyo kwa kuachana na makanjanja ili viheshimike kwa kutoa taarifa zenye kuzingatia maadili ya uandishi”, alisema Dkt. Mwakyembe.

Alifafanua kuwa katika kuadhimisha siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, kalamu ya mwandishi wa habari itetee ukweli na si mambo ya haramu kwa sababu ya siasa au rushwa ambayo huwa kichocheo cha uvunjifu wa amani.

Aidha aliitaka Idara ya Habari (MAELEZO) kuwa na utaratibu wa kukutana na wahariri kila mwezi ili kuweza kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili tasnia nzima ya habari nchini. Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Dkt. Hassan Abbasi alisema uandishi wa habari si biashara ya kawaida bali ni kazi yenye kuhitaji uweledi mkubwa hivyo waandishi wanatakiwa kufuata taratibu na sheria za uandishi.

SERIKALI YATOLEA UFAFANUZI SUALA LA VYETI FEKI

WAZIRI LUKUVI AMTUMBUA OFISA MIPANGO MIJI LINDI

$
0
0


Na  Hassan Mabuye & Muhammad Salim

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi ameamuru kusimamishwa kazi Afisa Mipango Miji wa Lindi Ndugu Castory Manase Nkuli baada ya kunyang`anya ardhi ya vijiji vya Ruvu na Mchinga hekari 4000 na kumilikisha kampuni ya Azimio Housing Estate kinyume cha sheria ya Ardhi.
Mhe. Lukuvi aligundua hayo baada ya kuona utaratibu wa umilikishaji wa ardhi haukufuatwa na badala yake kuonekana kuwa na mianya ya rushwa kwa kuwa ardhi hiyo imehamishwa kutoka ardhi ya kijiji hadi kumilikishwa kwa kampuni ya Azimio ambapo kisheria ilitakiwa hati ya eneo hilo itoke kwa idhini ya Rais.
Aidha, Afisa Mipango Miji huyo aligundulika kuwa na kosa la kughushi kwa kujifanya ni Ofisa ardhi baada ya kuandika barua na kuisaini kwa niaba ya Afisa ardhi wakati yeye ni Ofisa Mipango Miji ili kuimilikisha kampuni ya Azimio Housing Estate ambalo pia ni kosa kisheria.
Akithibitisha makosa hayo Kaimu Mkurugenzi Mipango Miji na Vijiji kutoka Wizara ya Ardhi  Immaculate Senje amesema kwamba utaratibu wa umilikishaji wa ardhi hiyo haukufuatwa ambapo kisheria ilitakiwa hati ya eneo hilo itoke kwa idhini ya Rais na baada ya Tangazo la Serikali na kuridhiwa na wana kijiji.
“Kama nyie hamna uwezo wa kumfukuza kazi basi mie namsimamisha kazi kuanzia leo hafai kuwa mtumishi wa serkali” alisema  Lukuvi na kuagiza eneo hilo lirudi na kuwa mali ya serikali “ Sasa hiyo ardhi lazima irudi itakua mali ya serikali kuanzia leo”  katika ziara hiyo,  Lukuvi ametembelea ofisi za ardhi Lindi na kufanya ukaguzi katika Masijala za ardhi na kuangalia mfumo wa ukusanyaji kodi ya pango la ardhi, kisha kuwaagiza watendaji wa ardhi mkoani hapa kuhakikisha wanatoa hati kwa wakati na kukusanya kodi ya pango la ardhi kwa kila mmiliki wa ardhi ili kuongeza pato la serikali. Pia alitembelea ofisi za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Mkoani hapa na kupokea taarifa kutoka kwa Meneja wa shirika hilo mkoani Lindi  Gibson Mwaigomole.
Katika taarifa hiyo  Lukuvi amelishauri Shirika la Nyumba la Taifa kufanya uwekezaji Mkoani Lindi kwa kujenga ofisi za kisasa pamoja na Nyumba zenye gharama nafuu.
Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Lindi Godfrey Zambi akiwa pamoja na waziri Lukuvi na watendaji wa mkoa ameeleza kuwa sekta ya ardhi mkoani hapo inachangamoto nyingi lakini ofisi yake inaendelea kufanya jitihada za makusudi kuhakikisha changamoto hizo zinapungua au kuzimaliza kabisa kwa maslahi ya watu wa Lindi na Tanzania kwa ujumla.

WAZIRI MWAKYEMBE AMPONGEZA RAIS MAGUFULI KWA KUTUMIA LUGHA YA KISWAHILI KAMA UTAMBULISHO WA KITAIFA


NKAMIA AKIMPONGEZA RAIS MAGUFULI KWA KUWA KIONGOZI MZURI

ATCL KUPATA NDEGE MPYA JULAI MWAKA HUU

$
0
0

Na Vicent Tiganya  Tabora

Serikali imesema kuwa mwezi Julai mwaka huu (2017)itanunua ndege nyingine mpya aina ya Dash 8-Q 400 kwa ajili kuliimarisha Shirika la Ndege la Tanzania ili liliweze kutoa kutoa huduma za usafiri wa anga katika maeneo mengi ndani na nje ya nchi.

Hatua hiyo itaiweza ATCL kufikisha ndege nne (4) ambapo itaiwezesha kuongeza safari zake kwa kuhudumia masoko yake ya ndani na miji ya nchi jirani kama vile Kenya, Uganda, Burundi , Rwanda, Malawi, Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC).

Kauli hiyo imetolewa jana na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasilano Mhandisi Edwin Ngonyani wakati wa uzinduzi wa Safiri za Ndege za Shirika la ATCL mkoani Tabora.

Alisema kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa hadi kufikia Julai mwakani (2018)Shirika la Ndege hapa nchini linakuwa na uwezo wa kumiliki Ndege sita zenye uwezo wa kubeba abira kwa kiwango tofauti tofauti na kusafiri mikoa mingi hapa nchi na nje ya Tanzania.

Naibu Waziri huyo alisema kuwa hadi hivi sasa , serikali imeshanunua ndege mbili aina ya Bombardier Dash 8-Q400 zenye uwezo wa kubeba abiria 76 kila moja.

Alisema kuwa hatua inayofuata ni ununuzi wa ndege nyingine tatu aina ya Bombardier Dash 8-Q400 ambayo itakuwa na uwezo kubeba abiria 76, CS 300 mbili zitakazobeba abiria 132 kila moja na Boeing 787 (Dreanliner ) itakayokuwa na uwezo wa kubeba abiria 262.

Aidha  Ngonyani alisema kuwa lengo la Serikali ya Awamu ya Tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kuhakikisha inaimarisha viwanja vya ndege kwa kukarabati miundombinu na kuboresha mifumo mbalimbali ya huduma za usafiri wa anga.

Alisema kuwa hatua hiyo inaenda sanjari uimarishaji wa Shirika la Ndege hapa nchini na ujenzi wa viwanja vipya vya ndege katika mikoa ambayo haina viwanja hivyo kwa sasa.

Ngonyani alisema kuwa Serikali kupitia Shirika lake imekusudia kuhakikisha kuwa mikoa yote hapa nchini inaunganisha na usafiri wa anga.

Alitoa wito kwa kwa wananchi kutumia usafiri wa anga hasa wa Shirika hilo kama huduma ya kawaida na ya kuongeza fursa ya kibiashara kwa ajili kuimarisha kipato kuanzia ngazi ya familia hadi taifa.

Ngonyani aliwaomba wakazi wa Tabora na maeneo mengine hapa nchini kutumia huduma za usafiri wa anga katika kutanua wigo wa biashara zao na kuhamasisha utalii na kuimarisa sekta ya kilimo cha kisasa hapa nchini.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi) Dkt. Leonard Chamuriho alisema kuwa Shirika la Ndege hapa nchini linatoa huduma nafuu ukilinganisha na mashirika mengine yanayotoa huduma hiyo hapa nchini.

Alisema kuwa lengo ni kuhakikisha kuwa wananchi wanatumia usafiri huo na kutokuwa wa watu wachache kama yalivyo mashirika mengine hapa nchini. Dkt. Chamuriho alisema kuwa Shirika hilo linatoza gharama nafuu ukilinganisha na Kampuni nyingine zinazotoa huduma za usafiri wa anga hapa nchini.

Alisema kuwa hivi sasa kutoka Dar es salaam kwenda Tabora kwa safari mmoja ni shilingi 330,000 na kutoka Tabora kwenda Dodoma ni shilingi 250,000  Dkt. Chamuriho aliongeza kuwa safari ya kwenda na kurudi kutoka Dar es salaam kwenda Tabora kwa safari mmoja ni shilingi 499,000 na kutoka Tabora kwenda Dodoma ni shilingi 380,000.

Wabunge wa Mkoa wa Tabora na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamemshuru Rais Dkt.John Pombe Magufuli kwa kutimiza ahidi yake kwa vitendo kwa kuanza kiliimarisha upya Sherika la Ndege hapa nchini.

Waliomba Serikali kupitia Shirika la ATCL kuendelea kupunza nauli za usafiri wa ndege ili wananchi wengi waweze kutumia usafiri wa anga hasa kupitia Shirika lao.

Wamesema kuwa haitakuwa na maana kama nauli zitakuwa juu na wananchi kuona usafiri wa anga ni watu matajiri tu.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Tabora  Aggrey Mwanri ametoa wito kwa wawekeza popote ndani na nje ya nchi kwenda mkoani humo kuwekeza katika sekta mbalimbali ikiwemo ya kilimo kufuatia kuimarika kwa miundo mbinu mbalimbali ikiwemo usafiri wa anga, barabara na mawasiliano ya simu.

Alisema kuwa Tabora inayoa ardhi nzuri inayokubali ufugaji na ukilima wa mazao mbalimbali kama vile tumbaku, mahindi, alizeti mbunga, karanga miazi, mihogo na mengine mengine hatu inayowezo kuwawezesha kufunga viwanda vidogo na vikubwa. Kwa mujibu wa ratiba ya safari za ndege za Shirika hilo mkoani Tabora zitakuwa Jumatau, Jumatano Ijumaa na Jumapili.

BURIANI MWANAHABARI REVOCATUS BULIZYA

$
0
0
Marehemu Revocatus Bulizya enzi za uhai wake
Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Mwanahabari Revocatus Bulizya wakati ukiingizwa katika Kanisa la Katoliki Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya ibada ya kuuaga kabla ya kwenda kwenye mazishi yaliyofanyika Mwandege Kongowe Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam leo.
Mjane wa marehemu na mtoto wao (katikati), akisaidiwa na dada yake aliyewahi kuwa Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Mkoa wa Dar es Salaam toka mwaka 2010/2015, Shelymar Kweygia kuingia katika kanisa hilo kwa ajili ya ibada ya kuuaga mwili huo.



Jeneza likiingizwa kanisani.


Waombolezaji wakiwa katika ibada ya kuuaga mwili huo.
Wanahabari wa Sahara Media alikokuwa akifanya kazi marehemu katika Kituo cha Televisheni cha Star TV na ndugu jamaa wa marehemu wakiwa kwenye ibada hiyo. 
Wanahabari wakiandika wasifu wa marehemu Revocatus Bulizya.
Wanahabari Kibwana Dachi (kulia) na Ben Mwanantala 
wakiwa kwenye ibada hiyo.
Katekista wa Parokia ya Muhimbili akiongoza ibada hiyo.
Ni huzuni katika ibada hiyo.

Na Dotto Mwaibale

VILIO na majonzi vilitawala wakati wa ibada ya kuuaga mwili wa mwanahabari Revocatus Bulizya wa Kituo cha Televisheni cha Star TV wakati wa ibada ya kumuaga iliyofanyika Kanisa Katoliki la Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) Dar es Salaam leo asubuhi.

Ibada hiyo ilihudhuriwa na ndugu jamaa na marafiki wa marehemu pamoja na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali akiwepo aliyewahi kuwa Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Mkoa wa Dar es Salaam toka mwaka 2010/2015, Shelymar Kweygia ambaye ni ndugu ya mke wa Bulizya.

Akitoa mahubiri wakati wa ibada hiyo Katekista wa Paroko ya Kanisa Katoliki MNH, alisema ni wakati wa kila mmoja wetu kutafakari juu ya maisha yake ya kimungu.

Alisema hakuna njia ya kukutana na mungu bila ya kifo na ndio maana wakati wote tunatakiwa kujiandaa kwa sababu hatui ni lina tutatoweka duniani kama alivyotuacha ndugu yetu Revocatus Bulizya.

Recocatus Bulizya alzaliwa tarehe 29-10-1979 na kufariki dunia tarehe 2-5-2017 kwa kugongwa na pikipiki 'bodaboda' maeneo ya Pugu jijini Dar es Salaam wakati akirejea nyumbani kwake akiwa ameongoza na mke wake.

Mazishi ya marehemu yamefanyika Mwandege Kongowe Barabara ya Kilwa nje kidogo ya jijini Dar es Salaam na mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu.

RC GAMBO AWALILIA WATOTO 32 WALIOFARIKI KWA AJALI KARATU

$
0
0

Pichani wanafunzi wakisubiri basi kabla ya kuanza safari ambapo walikutwa na mauti

Mwanafunzi mmoja aliyenusurika kwenye ajali hiyo  jina halikufahamika.
Mzazi wa mmoja wa marehemu akilia kwa uchungu.

Baadhi ya watu wakishuhudia basi hilo likiwa limetumbukia  kwenye bonde,pia wakitoa msaada,
Baadhi ya miili ya wanafunzi hao walifariki  kwenye ajali hiyo.
Hili ni kati ya mabasi ya shule hiyo ya Lucky Vincent  lililokuwa kwenye msafara huo.
Blog hii inatoa mkono wa pole  kwa wazazi wote wa marehemu waliopiteza watoto wao, Mungu azilaze roho zote  mahala pema peponi Amin.

MAKAMU WA RAIS MAMA SAMIA SUKUHU HASSAN KUONGOZA KUAGA MIILI YA WANAFUNZI 32

Viewing all 1934 articles
Browse latest View live