Quantcast
Channel: BONGOWEEKEND
Viewing all 1941 articles
Browse latest View live

TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI YAFAFANUA HATMA YA UBUNGE WA SOFIA SIMBA

$
0
0


****************************************************
Tume ya Taifa ya Uchaguzi inapenda kuutarifu Umma kuwa; kwa mujibu wa Kifungu cha 37 (3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343, Mhe. Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemjulisha Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa; kufuatia Mbunge wa Viti Maalum, Sophia Mnyambi Simba kufukuzwa uanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) tarehe 11 Machi, 2017 kiti cha Mbunge huyo wa Viti Maalum Wanawake kwa tiketi ya CCM kiko wazi.
 Kwa mujibu wa Ibara ya 67 (1) (b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ili mtu ateuliwe au achaguliwe katika nafasi ya Ubunge ni lazima awe mwanachama aliyependekezwa na Chama chake husika cha Siasa.

Kwa kuwa  Sophia Mnyambi Simba amefukuzwa uanachama wa Chama kilichomdhamini, Ibara ya 67 (2) (e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inaelekeza kuwa Mbunge huyo amepoteza sifa za kuteuliwa au kugombea Ubunge.
Kutokana na kuwepo kwa nafasi wazi ya Ubunge wa Viti Maalum, taratibu za kujaza nafasi hiyo zinaendelea kwa kuzingatia kifungu cha 86A (8) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343.


Jaji (R) Semistocles Simon Kaijage
Mwenyekiti
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

12  Aprili, 2017

RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA RELI YA KISASASTANDARD GAUGE DAR HADI MOROGORO

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia kibao cha jiwe la msingi cha Ujenzi wa Reli ya Kisasa Standard Gauge itakayoanzia jijini Dar es Salaam hadi mkoani Morogoro na baadaye kuendelea hadi Kigoma na Mwanza.
Uzinduzi huo umeshuhudiwa na  Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mabarawa, Mama Janeth Magufuli na Mkurugenzi  Mtendaji wa RAHCO Masanja  Kadogosa.

Viongozi wengine waluoshuhudia  ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaa Paul Makonda Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Miundombinu Profesa Norman Sigala , Hawa  Ghasia (Mb) na Mufti Mkuu wa Tanzania Shekhe Abubakary Zubeiry .(PICHA NA IKULU).
         

Na  Immaculate Makilika- MAELEZO

Tanzania inatarajiwa kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kuwa na reli ya kisasa inayotumia umeme na mafuta itakayokuwa na uwezo wa kusafiri  masafa marefu kwa mwendokasi wa kilometa 160 kwa saa.

Akizungumza leo katika uwekaji wa jiwe la msingi wa awamu ya kwanza ya ujenzi wa reli hiyo ya leo huko Pugu nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alisema kuwa reli hiyo itakuwa ya kisasa zaidi barani Afrika na itasaidia kukuza uchumi wa nchi kwa kuchochea fursa za biashara ndani na nje ya nchi.

Awamu ya kwanza ya ujenzi wa reli hiyo ambayo itahusisha kipande cha kilomita 300 kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro utagharimu jumla ya shilingi trilioni 2.8 na utatarajiwa kukamilika katika kipindi cha miezi 30.

Dkt Magufuli alitoa mfano wa nchi zenye reli za mwendokasi lakini masafa mafupi barani Afrika kuwa ni Morocco ambayo inasafiri kwa mwendokasi wa kilomita 220 kwa saa na Afrika Kusini inayosafiri mwendokasi 150 kwa saa.

Dkt Magufuli alieleza kuwa baada ya kukamilika kwa mradi huo Tanzania itakuwa nchi ya kwanza kuwa na treni itakayosafiri masafa marefu kwa mwendokasi wa km 160 kwa saa.

Alifananua kuwa mradi huo wa ujenzi wa reli unatekelezwa kwa fedha za Tanzania ambapo tayari serikali imeshawalipa wakandarasi malipo ya awamu ya jumla ya shilingi bilioni 300.

Akizungumzia umuhimu wa ujenzi wa reli hiyo, Rais Magufuli alisema kuwa reli hiyo itasaidia kuongeza kasi ya usafirishaji wa mizigo kutoka bandari ya Dar es Salaam kwa haraka na kuwafikia wateja ndani ya muda mfupi.

Vilevile, reli hiyo itarahisisha usafirishaji wa abiria na mizigo pamoja na kukuza biashara kati ya Tanzania na nchi jirani za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC, Uganda, Burundi, Rwanda na Sudani ya Kusini.

Sambamba na hayo, Rais Magufuli alisema kuwa ujenzi wa reli hiyo utasaidia kuimarisha sekta nyingine za uchumi ikiwemo utalii, viwanda, kilimo, pamoja na kutoa ajira kwa watanzania ambapo kutakuwa na ajira muda zipatazo 600,000, na ajira za kudumu 30,000.

Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa alisema kuwa reli hiyo ya kisasa inayojengwa na wakandarasi kutoka muungano  wa kampuni mbili za nchi ya Uturuki na  Ureno  itakuwa na uwezo wa kusafirisha mizigo tani 10,000 kwa mara moja  na kutumia saa 2 kutoka Dar es salaam hadi Dodoma na saa 7 na dakika 40 kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza.

Naye, Mjumbe wa Bodi ya Kampuni ya ujenzi kutoka Uturuki ya Yapi Merkezi Bw.  Emre Aykar alisema kuwa reli hiyo itaimarisha zaidi uhusiano wa Uturuki na Tanzania na kuongeza kiwango cha shughuli za biashara nchini.

“Tunaahidi kujitahidi kumaliza mradi kwa wakati na katika kiwango kinachotakiwa” alisema Bwana Aykar.

Reli hiyo ya kisasa inatarajiwa kujengwa pembeni ya reli ya kati ambayo ilijengwa wakati wa utawala wa kikoloni wa Wajerumani na Waingereza miaka 112 iliyopita.

                           

SERIKALI KUFANYA MAREKEBISHO SHERIA YA NDOA YA MWAKA 1971

$
0
0

Na Daudi Manongi-MAELEZO, Dodoma

Serikali kupitia Wizara ya Katiba na Sheria imesema inaendelea na mchakato wa ndani wa kufanyia marekebisho ya kuhuisha na kuimarisha maeneo yaliyo mazuri ya sheria ya ndoa ya mwaka 1971 na kuwasilishwa Bungeni ili kuendana na wakati.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Prof.Palamagamba Kabudi wakati akijibu hoja mbalimbali za wabunge Mjini Dodoma.

“Serikali inaendelea na mchakato huu wa mapendekezo ya marekebisho ya Sheria hii Bungeni ili iweze kuendana na wakati kwa kuondoa upungufu uliopo kwa maslahi mapana ya nchi yetu”,Aliongeza Mhe.Kabudi.

Amesema kuwa baada ya miaka 20 kupita tangu sharia hiyo ya ndoa itungwe,Serikali kupitia tume ya kurekebisha Sheria iliifanyia mapitio ya sheria hiyo na kubaini maeneo kadhaa yenye udhaifu na hivyo kuhitaji kufanyiwa marekebisho.

Amebainisha kuwa Kutokana na maoni hayo ya tume,mwaka 2008 Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria iliandaa waraka wa baraza la Mawaziri uliokuwa na mapendekezo ya marekebisho ya sharia ya ndoa ya mwaka 1971,hata hivyo desemba 2010 kabla waraka huo kujadiliwa na kuridhiwa na baraza la Mawaziri mchakato wa mabadiliko ya katiba ya jamhuri ya muungano ukaanza na kulilazimu Baraza kusitisha kwa muda mchakato huo.

“Serikali ilikuwa na matarajio kuwa wakati tume ya mabadiliko ya katiba inakusanya maoni ya wananchi kuhusu mabadiliko ya katiba,wananchi wangetoa maoni kuhusu Sheria ya ndoa pamoja na sheria nyingine zinazofanana na hiyo na hivyo maoni yaliyotolewa wakati wa Sheria ya Ndoa yalikuwa machache sana”Alifafanua Mhe.Kabudi. Sheria ya ndoa mwaka 1971 ni matokeo ya mjadala mpana na shirikishi kupitia waraka wa Serikali namba moja wa mwaka 1969.

TASNIA YA HABATI YAPATA PIGO, ISANGO AMEFARIKI DUNIA LEO

$
0
0
Mwanahabari Josephat Isango amefariki  dunia  leo saa moja asubuhi Mkoani Singida baada ya kuumwa kwa muda mfupi.

Marehemu Isango atakumbukwa  kutokana na mchango wake mkubwa katika uandishi wa habari za siasa   na  jamii kwa ujumla.Nyota ya fani ya uanahabari ilishamiri alipokuwa ameajiriwa na Kampuni ya Free Media Limited ambao ni Wachapishaji wa gazeti la Tanzania Daima na baadaye alihamia gazeti la Mwana halisi.Mazishi ya Isango yatafanyika  Jumamanne  Mkoani Singida.

RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI MAUAJI YA ASKARI 8 KIBITI MKOANI PWANI

DAWASA UKINGONI KUKAMILISHA KAZI

$
0
0


Mafundi wa TANESCO wakiwa kwenye ukaguzi katika eneo la Chalinze (Sub-station) ambapo laini ya umeme unaoelekea katika mtambo wa Ruvu Juuinapoanzia.

Mtaalam wa Kitengo cha Umeme Mkubwa wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Emmanuel Haule (kushoto) akikagua mitambo mipya inayotarajiwa kupokea umeme na kutembeza pampu mpya.



Mafundi wakiwa kazini kuunganisha nyaya toka katika laini ya umeme inayotoka Chalinze (Sub-station) na kuiingiza katika laini ya Ruvu Juu ili iweze kuongeza nguvu ya umeme kwa ajili ya kuzalisha maji zaidi.

Hii ni Transfoma mpya iliyopo katika eneo la Mtambo wa Ruvu Juu ambalo kwa sasa linafanya kazi vizuri ya kutoa umeme kwa ajili ya mitambo.

Mtambo mpya wa kusukuma maji wa Ruvu Juu kama unavyoonekana, mtambo huu unafanya kazi vizuri ya kusukuma maji.

Hii ni sehemu ya mtambo wa kuwashia na kuongoza mitambo inayofanya kazi ya kusukuma maji eneo la Ruvu Juu kama unavyoonekana.

Hili ni eneo la mtambo wa maji wa Ruvu Juu ambapo maji husafishwa na kisha kupelekwa katika mtambo mwingine kwa usafishaji zaidi na kisha kusafirishwa kwa wananchi.

Hili ni jengo la Utawala la Ruvu Juu ambapo shughuli za masuala ya maji zinafanywa na watendaji wake.

Hili ni eneo la mtambo wa maji wa Ruvu Juu ambapo maji yaliyosafishwa toka mitamboni hupitia ikiwa ni hatua ya mwisho tayari kusafirishwa kwenda kwa wananchi.

Hili ni bomba kubwa la maji safi la Ruvu Juu ambapo maji yaliyosafishwa toka mitamboni hupitia na kupelekwa sehemu ya kuyasafirisha kwenda kwa wananchi.


Hili ni eneo la mtambo wa maji wa katika eneo la IN TAKE lililopo katika Mto Ruvu na ndiyo sehemu maji hunyonywa na mitambo na kuyapeleka eneo la Ruvu Juu kwa ajili ya kusafishwa.

Hii ni sehemu ya mtambo wa kuwashia na kuongoza mitambo inayofanya kazi ya kusukuma maji eneo la IN TAKE lililopo Mto Ruvu.

Hii ni mitambo ya kusukuma maji iliyopo katika eneo la IN TAKE katika eneo la Mto Ruvu na ndiyo sehemu inayofanya kazi ya kukusanya na kusukuma maji kuelekea Ruvu Juu.

Hili ni jengo la IN TAKE ambapo ndani ndipo iliposimikwa mitambo inayotumika kusukuma maji kuelekea eneo la Ruvu Juu kwa ajili ya kusafishwa na kusambazwa kwa wananchi.

Hili ni Transfoma kubwa lenye uwezo wa 45/55 MVA na ndiyo linalotoa umeme kupeleka eneo la Ruvu Juu kwa ajili ya kusukuma maji.

Nguzo unazoziona upande wa kulia kwa mbali ndiyo laini ya umeme ilipopita kutoka katika Transfoma inayotoa nguvu ya umeme ya 45/55 MVA, hivyo nyaya za umeme zimepitishwa chini kuelekea katika nguzo hizo zinazoonekana ambazo nazo husafirisha umeme huo kwenda Ruvu Juu.

(PICHA/HABARI NA MWANDISHI WETU)



KAZI ya ujenzi wa laini mpya ya umeme wenye nguvu ya 33KV kutoka Chalinze (Sub-station) kwenda Mlandizi yenye urefu wa kilomita 45 kwa lengo la kuongeza umeme ili kukidhi mahitaji ya upanuzi wa mtambo uliofanyika na kuweza kusukuma ujazo wa lita za maji milioni 196 kwa siku sasa umekamilika na majaribio ya matumizi ya laini hiyo yameanza kwa matarajio ya kukamilisha kazi hiyo ndani ya siku mbili.

Taarifa ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) ilifafanua kwamba, DAWASA kupitia Mkandarasi wake M/s WABAG kutoka nchini India kwa kushirikiana na Mkandarasi Msaidizi, Kampuni ya M/s Mollel Electrical Contractors ya hapa nchini kwa sasa wamemaliza kazi zote za ujenzi wa laini kutoka Chalinze mpaka eneo la kuingizia umeme ndani ya Mtambo wa Maji wa Ruvu Juu uliopo Mlandizi tayari kwa majaribio ya awali ya kiusalama na kuwasha pampu.

Mtambo huo wa maji wa Ruvu Juu utakua ukipokea umeme wa kutosha kutoka katika transfoma kubwa iliyopo kituo kidogo cha umeme Chalinze (Sub-station) yenye uwezo wa 45/55 MVA ambapo itawezesha pampu zote mpya zilizofungwa kuwashwa. 

Hapo awali mtambo huo ulikuwa na uwezo wa kuzalisha lita milioni 82 kwa siku na mara baada ya majaribio haya na kuongeza umeme ndani ya siku mbili uzalishaji wake utaongezeka kufikia lita milioni 196 kwa siku.

Taarifa ya DAWASA inabainisha kuwa, ili lita hizo milioni 196 za maji ziweze kusukumwa na mtambo huo wa Ruvu Juu, mtambo unahitaji 16MVA za umeme ili kusukuma maji safi yanayozalishwa baada ya upanuzi kwa asilimia100.

Aidha, Mkandarasi kwa sasa amekamilisha kazi ya kujenga laini hiyo mpya toka sub-station ya Chalinze ikiwa ni pamoja na kazi zote zilizotakiwa kufanyika ndani ya kituo hicho kidogo cha umeme cha Chalinze. Hizo ni pamoja na kazi mbalimbali zilizotakiwa kufanyika ili kuweza kuupokea umeme huo kutoka kwenye transfoma hiyo.

Aidha, maeneo nufaika ya mtambo wa maji wa Ruvu Juu ni Mkoa wa Dar es Salaam, mkoa wa Pwani, maeneo ya mji wa Mlandizi, Kibaha na baadhi ya Vitongoji vyake.

DAWASA inaendelea kulishukuru Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa ushirikiano na ushauri wa kitaalam kuhusiana na masuala ya umeme ambao imekua ikiutoa mara kwa mara ili kuhakikisha kuwa maji ya kutosha yanapatikana katika jiji la Dar es Salaam na maeneo yote yanayohudumiwa na DAWASA.

Mikataba ya upanuzi wa mtambo na ujenzi wa mabomba mapya kutoka Ruvu Juu mpaka Kimara pamoja na ujenzi wa tanki kubwa lenye ujazo wa lita million 10 ilisainiwa mwaka 2014 na Serikali kupitia Wizara ya Maji na Umwagiliaji ilipata fedha hizo kwa mkopo wa masharti nafuu toka Benki ya Exim ya India.

Article 2

ASKOFU DKT.ALEX MALASUSA AONGOZA IBADA YA IJUMAA KUU KANISA LA KKKT USHARIKA WA AZANIA FRONT JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 Muumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Azania Front, Moses Kombe (katikati) na wenzake wakiigiza igizo la kumbukumbu ya kuambwa msalabani kwa Yesu Kristo miaka 2000 iliyopita katika ibada ya Ijumaa Kuu iliyofanyika katika kanisa hilo jijini Dar es Salaam leo jioni.
 Igizo likiendelea.
 Askofu mstaafu Dk. Alex Malasusa akisalimiana na waumini wa kanisa hilo baada ya ibada ya Ijumaa Kuu.
 Muonekano wa waumini wakati wa ibada hiyo.
 Kwaya Kuu ya Ushairika huo ikitoa burudani ya nyimbo za kifo chake Yesu Kristo wakati wa kuhitimisha ibada hiyo.
 Waumini wa kanisa hilo wakiwa nje kwa kuhitimisha ibada hiyo.
Waumini wakitakiana kheri ya Ijumaa Kuu baada ya ibada hiyo.

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAANZA KUKUSANYA MAONI KUTOKA KWA WADAU WA UTALII

$
0
0
Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imewataka wadau wa Utalii nchini kutoa maoni na michango yenye tija itakayopelekea upatikanaji wa Sera bora itakayoleta ufanisi katika uendeshaji wa huduma zinazotolewa katika sekta ya Utalii.

Hatua hiyo inakuja ikiwa, Sera ya Taifa ya Utalii iliyopo ilifanyiwa mapitio kwa mara ya mwisho mwaka 1999 ambapo ni takribani miaka 17 iliyopita.

Katika kutambua hilo, Wizara imeanza kupitia upya Sera hiyo ili kuhakikisha Sekta ya Utalii inakwenda sambamba na mabadiliko mbalimbali yanayotokea duniani yakiwamo ya teknolojia, kijamii, kiuchumi, kisiasa na mazingira akizungumza katika mkutano unaofanyika kwa muda wa siku mbili Jijini Arusha kwa mikoa ya kanda ya Kaskazini, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki alisema Sera inafanyiwa marekebisho kwa kuwa imepitwa na wakati kutokana na mabadiliko makubwa yaliyotokea katika sekta hiyo.

Aidha, alisema kwa kutambua mchango wa utalii kiuchumi , ni wazi kuwa sera wezeshi ya utalii yenye kutoa mwongozo wa utaratibu bora na sahihi wa usimamizi, uendelezaji na utendaji katika sekta hiyo unahitajika.

’’ Tunataka kuibadilisha sera hiyo ili iweze kujibu changamoto za aina ya utalii wa sasa ambao kipindi cha nyuma haukuwepo, akitolea mfano utalii mikutano pamoja na utalii wa kiutamaduni ambao umekuwa ukikua kwa kasi hapa nchini. Kutokana na hali hiyo, Dkt. Nzuki amesema marekebisho ya Sera hiyo yanahitaji mchango mkubwa kutoka kwa wadau kwa kuwa inaendeshwa kwa kiasi kikubwa na Sekta Binafsi katika kutoa huduma na kufanya biashara za utalii hapa nchini.

Awali, Mkurugenzi wa Idara ya Utalii, Zahoro Kimwaga alisema uhuishwaji wa Sera hiyo utazingatia namna ambavyo wazawa wataweza kuwa wanufaika namba moja kwa kuwaandalia mazingira rafiki ya kuendesha biashara ya utalii tofauti na sasa ambapo makampuni mengi ya utalii ni ya watu kutoka nje.

Naye, Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Utalii Tanzania, Richard Lugimbana alisema sera iliyopo sio mbaya ila tatizo lililopo Serikali imeshindwa kuitekeleza licha ya kuwa kuna baadhi ya vitu muhimu ambavyo havimo kwenye sera hiyo ikiwemo changamoto za mabadiliko ya tabia ya nchi.

Aliongeza kuwa mara baada ya kuhuisha sera hiyo itaweza kusaidia kuonesha jinsi gani wadau wa utalii wanayokumbana na changamoto mbalimbali katika kuwahudumia watalii. Kwa upandwe wa Mwenyekiti wa TATO, Wilbert Chambulo alisema suala la kuifanyia marekebisho ya sera hiyo ni jambo jema ila sasa serikali iangalie namna ya kuboresha mashirikiano katika utoaji wa maamuzi kwa wafanyabiashara wa utalii nchini badala ya kuamua yenyewe pekee yake Mkutano huo wa kukusanya maoni kutoka kwa wadau umeanza kufanyika Mkoani Arusha kwa kuwashirikisha wadau kutoka mikoa minne ya Kanda ya Kaskazini na badaaye utafanyika katika kanda zingine kwa muda wa siku mbili mbili kwa ushirikiano kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Shirikisho la Vyama Vya Utalii Tanzania (TCT) pamoja na Benki ya Dunia chini ya uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu .

DUKA LA KISASA LA GSM MALL LAUNGUA MOTO

$
0
0
 Magari ya Zimamoto na Uokoaji yakiwa nje ya Duka kubwa la GSM Mall tayari kuzima moto uliokuwa unaunguza duka hilo katika Barabara ya Nyerere eneo la Mtava, Dar es Salaam. Chanzo cha moto huo hakikuweza kujulikana mara moja. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Mmoja wa majeruhi wa ajali hiyo akiwahishwa hospitali.
 Pilikapilika katika lango kuu la kuingilia duka hilo

 Mmoja wa majeruhi akitolewa kwenda kwenye gari ili awahishwe hospitali kwa matibabu
Wananchi wakishuhudia ajali hiyo ya moto


Na Richard Mwaikenda 

DUKA kubwa la GSM Mall ililopo Barabara ya Nyerere eneo la Mtava, Dar es Salaam, linateketea kwa moto hivi sasa.

Kwa mujibu wa mashuhuda ni kwamba duka hilo lilianza kuungua majira ya 8;30,hadi sasa chanzo cha moto huo hakijaweza julikana. 

Magari ya zimamoto na uokoaji yamejazana eneo hilo kunusuru mali na maisha ya watu waliokuwemo kwenye jengo hilo lenye ghorofa nne.

Watu wengi wakiwemo wafanyakazi wa duka hilo walionekana kutoka mkuku kuokoa maisha yao.

 Baadhi yao walitolewa wakiwa mahututi na kukimbizwa hospitali kwa kutumia magari ya polisi.

Duka hilo kubwa la kisasa lenye maduka yenye aina mbalimbali za bidhaa ni moja kati ya maduka makubwa yaliyopo jijini Dar es Salaam.

Waokoaji waliokuwepo wamepata wakati mgumu kuzima moto kutokana na ndani ya jengo hilo kuwa na giza nene lililotawaliwa na wingu la moshi uliosababishwa na moto huo.

Wamejitahidi kupata mwanga kwa kuwasha taa za magari karibu na lango kuu la kuingilia ndani lakini ilishindikana.

RAIS MAGUFULI AAGIZA TCU KUTOWACHAGULIA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU VYUO

$
0
0


Na Lilian Lundo na Beatrice Lyimo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameiagiza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kutowachagulia vyuo wanafunzi wa elimu ya juu na kuwaacha wanafunzi hao kuchagua vyuo wanavyovitaka wenyewe.
Agizo hilo limetolewa leo, Jijini Dar es Salaam Rais Magufuli alipokuwa akizindua Mabweni mapya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ikiwa ni ahadi yake aliyoitoa Chuoni hapo Juni, mwaka jana.
“Ninaamini kama wanafunzi wangepewa nafasi ya kuchagua vyuo wanavyovipenda wenyewe, vyuo vya Serikali kama vile Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na Chuo Kikuu cha Mzumbe vingekuwa na wanafunzi wengi sana,” alisema Dkt. Magufuli.
Aliendelea kwa kusema kuwa TCU imekuwa ikiwachagulia wanafunzi vyuo visivyo na sifa na makazi ya wanafunzi hivyo kusababisha wanafunzi hao kusoma katika mazingira magumu na wanapomaliza masomo yao hukosa ajira kutokana na vyuo hivyo kutokuwa na sifa.
Aidha, Rais Magufuli ameuagiza uongozi wa UDSM kutoza wanafunzi gharama ya shilingi mia tano(500) kama malipo ya makazi ya mabweni hayo kwa siku badala ya shilingi mia nane(800) inayotozwa kwa mabweni mengine yaliyopo chuoni hapo.
Alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga kuwekeza katika elimu hivyo itahakikisha wanafunzi nchini wananufaika kwa kupata elimu bora kuanzia shule za msingi hadi vyuo vikuu.
“watanzania walinichagua ili kutatua changamoto zinazowakabili na hivi ndivyo ninavyofanya kutatua changamoto hizo” alisema Rais Magufuli.
Naye, Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amempongeza Rais Magufuli kwa kutoa shilingi bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni hayo ambao kwa kiasi kikubwa yatatatua changamoto ya makazi iliyokuwa ikiwakabili wanafunzi wa chuo hicho. Prof. Ndalichako amesema kuwa mabweni hayo yamejengwa kwa kipindi cha miezi 8 ambayo yatachukua wanafunzi 3840.
Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo cha Kikuu cha Dar es Salaam Prof. Rwekaza Mukandala ametoa rai kwa wanafunzi wa chuo hicho kuhakikisha wanaimarisha usalama katika maeneo ya mabweni hayo na kulinda miundo mbinu yote iliyoweka.
“Ni lazima mzingatie matumizi sahihi ya kila kifaa kilichofungwa katika majengo haya, majengo haya ni mapya na yamejengwa kwa gharama kubwa kwa lengo la kutusaidia kuondokana na changamato iliyotukabili kwa muda mrefu,” alisema Prof. Mukangala.
Wakati huohuo Rais Magufuli ameweka jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi magomeni “Quarters”, mradi ambao kwa asilimia kubwa unawagusa watanzania wa hali ya chini.
Aidha Rais Magufuli ameendelea kusisitiza juu ya ahadi aliyoitoa kwa wakazi 644 waliokuwa wakiishi maeneo hayo kupewa nyumba ambapo wataishi bure kwa muda wa miaka mitano.
Pia, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo (TBA) Msanifu Majengo Elvis Mwakalinga amesema ujenzi wa mradi huo umezingatia miundombinu yote iliyohitajika ambapo itakuwa na sehemu za makazi, biashara, maegesho ya magari na bustani ya kupumzikia. Ujenzi wa mradi huo unatarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha mwaka mmoja ambapo ujenzi wake ulianza rasmi Oktoba mwaka jana.

MIILI YA ASKARI NANE WALIOUAWA NA MAJAMBAZI KIBITI YAAGWA RASMI ,WAZIRI MWIGULU ATANGAZA KIAMA KWA WATUHUMIWA

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchini, Mwigulu Nchemba, akitoa heshima za mwisho Dar es Salaam leo mbele ya majeneza yenye miili ya askari nane waliouawa na majambazi Kibiti wilayani Mkuranga mkoani Pwani juzi jioni.Kulia kwake ni Naibu Waziri wa wizara hiyo, Masauni. (Picha zote na Dotto Mwaibale)

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchini, Mwigulu Nchemba, akitoa pole kwa wafiwa.
Ndugu,jamaa na marafiki wa wafiwa wakiwa katika shughuli hiyo ya kuaga miili ya wapendwa wao.
Maofisa wa Uhamiaji wakiwa kwenye shughuli hiyo.
Wananchi wakiwa katika shughuli hiyo ya uagaji wa miili hiyo.
Maofisa wa Polisi wakishiriki kuaga miili ya wenzao hao.
Foleni ya kuaga miili hiyo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchini, Mwigulu Nchemba (kulia), akiteta jambo na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Ernest Mangu wakati wa kuaga miili hiyo.
Mmoja wa ndugu za askari hao akilia kwa uchungu.

Ni kilio kwa kuwapoteza wapendwa wao.
Ni huzuni.

Na Dotto Mwaibale 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amewatangazia kiama watu wote waliohusika kuwaua askari polisi nane Kibiti wilayani Mkuranga mkoani 
Pwani.

Akizungumza wakati wa kuaga miili ya askari hao jijini Dar es Salaam leo asubuhi Mwigulu alisema watu hao watakamatwa  wote na kufikishwa kwenye mkono wa sheria.

"Kitendo hiki cha mauaji kilichofanyika dhidi ya askari wetu hakivumiliki hata kidogo waliohusika tutawatafuta na kuwakamata" alisema Mwigulu.

Aliwaomba wananchi wa maeneo husika kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kuwapata wahusika wa tukio hilo.

Katika hatua nyingine Mwigulu ameitaka wizara husika kuhakikisha inatoa fidia kwa ndugu wa askari hao na majeruhi badala ya kuchukua muda mrefu kuitoa.

"Naomba fidia kwa askari hawa tuliowapoteza wakitumikia taifa itolewa haraka bila kucheleweshwa" aliongeza Mwigulu.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Ernest Mangu alisema watuhumiwa wote waliohusika kufanya mauaji hayo ni lazima watafikiwa na mkono wa dola.

Alisema wananchi wa eneo hilo wanawafahamu wahusika hivyo amewaomba washirikiane na polisi ili kuwapata vinginevyo nguvu itatumika.

Alisema linapotokea tukio kama hilo kuna baadhi ya watu wamekuwa wakishabikia kupitia mitandao ya kijamii hivyo akatoa onyo kuwa watakao bainika na wao watakamatwa kwa kutenda kosa.

Askari waliopoteza maisha katika tukio hilo la kinyama wametajwa kuwa ni pamoja na Mkaguzi Msaidizi Peter Kiguu, Koplo Francis, PC Haruna, PC Jackson, PC Zakaria, PC Siwale, PC Maswi na PC Ayoub


MKURUGENZI JIJI ARUSHA ATOA SEMINA KWA WATUMISHI WAKE

$
0
0
 Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Athumani Juma Kihamia

Na Mwandishi Wetu, Arusha

Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Athumani Juma Kihamia amefanya kikao na watumishi wa serikali katika Kata ya Muriety na Terati na kuzungumza mambo mbalimbali ambayo yatasaidia kuboresha utendaji kazi wao.

Kihamia amesema kuwa lengo hasa la kuonana na watumishi hao ni muendelezo wa ziara yake ya kutembela kila Kata na kuwakumbusha watumishi hao jinsi ya kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya tano ya Raisi John Magufuli.

“Siyo kwamba watumishi wangu wa Halmashauri hawafanyi kazi bali ni kuwakumbusha majukumu yao katika kutumikia wananchi hasa katika kasi ya serikali ya awamu ya tano ya hapa kazi tu ambayo inatutaka tuwe karibu zaidi na wananchi wetu na mimi kama mtendaji mkuu lazima nisimamie kikamilifu alisema Kihamia.

Vile vile amesema kuwa watendaji wa serikali wanatakiwa wajitume kwa nguvu zote wasisubiri mpaka viongozi wa juu wafike kwenye maeneo yao na wananchi walalmike wakati kuna kiongozi katika eneo hilo ambaye analipwa na serikali ili kusaidia wananchi.

" Hatutaki  mwananchi atoke kwenye Kata mpaka kwa mkuu wa Mkoa au mkuu wa Wilaya wakati kwenda kumlalamikia masuala madogo madogo wakati kuna kiongozi ambaye tumemuweka ili atatue kero akitokea Mtumishi wa hivyo ajue kwamba hatoshi kuongoza wananchi ”alisema Kihamia

Ameongeza kuwa kwasasa anahakikisha Huduma zinaboreshwa katika jiji la Arusha kwa kumjengea mtumishi uzoefu wa kufanya kazi bila kuogopa changamoto zilizopo na kuwa jasiri wakati anaongoza wananchi kwenye maeneo yao.

Hata hivyo amewagiza watumishi hao wa serikali wakiwemo watendaji kutekeleza kwa muda uliowekwa mambo muhimu kama vikundi vya vijana na Wanawake, kuainisha maeneo ya biashara na idadi yake ikiwemo mabango na maduka yote,majengo na miradi viporo pamoja na kuainisha Yale maeneo yote ya wazi. 

RAIS MAGUFULI ATOA AJIRA KWA MADAKTARI 258 WALIOOMBA KWENDA KENYA

$
0
0

Na Daudi Manongi-MAELEZO, Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  John Pombe Magufuli ameamua madaktari 258 na wataalamu wa Afya 11 walioleta maombi na kukidhi vigezo kupitia Wizara ya Afya kwa ajili ya kwenda kufanya kazi nchini Kenya kuajiriwa na Serikali.
Hayo yamebainishwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.
“Kwa upande wetu sisi ratiba ya utekelezaji wa ajira hizi za madaktari hao ilikubalika na pande zote iwe tarehe 6 Aprili 2017 na Madaktari hao wawe tayari kusafiri kwenda nchini Kenya kati ya tarehe 6-10 Aprili 2017, hadi tarehe ya Taarifa hii Mahakama nchini Kenya haijaondoa pingamizi lililofunguliwa kuhusu Ajira za madaktari wa Tanzania nchini Kenya,” alisisitiza  Mwalimu.
Amesema kufuatia uamuzi huu majina ya Madaktari husika na vituo watakavyopangiwa kazi yatatangazwa katika Tovuti ya Wizara pamoja na wataalamu wengine wa afya 11 walioleta maombi yao na kukidhi vigezo.
Aidha Serikali ya Tanzania itakuwa tayari kushughulikia upya ombi la Serikali ya Kenya kupatiwa Madaktari 500, pale ambapo hakutakuwa na vikwazo vya kupeleka madaktari wetu nchini Kenya.
Mnamo tarehe 18 Machi 2017 Ujumbe wa Serikali ya Kenya ukiongozwa na Waziri wa Afya Dkt.Cleopa Mailu uliwasili nchini ambapo ulikutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli kwa madhumuni ya kuomba kuajiri kwa Mkataba Madaktari wa Tanzania mia tano(500) ili kupunguza uhaba wa Madaktari nchini Kenya na kukubali ombi hilo.
Aidha Maombi hayo yalipokelewa ambapo jumla ya maombi 496 yaliwasilishwa na baada ya kufanya uchambuzi wa maombi hayo ilibainika kuwa Madaktari 258 walikidhi vigezo vilivyotakiwa kwenda kufanya kazi nchini Kenya,lakini wakati Serikali ya Tanzania ikiendelea kukamilisha utaratibu wa ajira za Madaktari hao Madaktari watano wa Kenya waliwasilisha pingamizi mahakamani kuitaka Serikali ya nchi yao kusitisha kuajiri Madaktari kutoka Tanzania.

DAWASCO YAKAMILISHA UPANUZI WA MTAMBO RUVU JUU SASA WAZALISHA MAJI SAFI NA SALAMA LITA1962

$
0
0



Maji yakiingia toka katika mitambo ya kunyonya maji tayari kwa kusafishwa kwa kuweka dawa ndani ya eneo hili na kisha kupelekwa katika mtambo mwingine wa kusafisha maji tayari kwa kusafirishwa.
Mtambo huu ni sehemu ambapo maji huendelea kusafishwa na kisha kupelekwa katika mtambo maalum wa kukusanya na kusafirisha kwenda kwa wananchi.

Matanki makubwa ya maji yenye mitambo maalum ya kusafisha maji kama inavyoonekana hapa maji  yakiendelea kusafishwa.

Sehemu hii ni ya mtambo ambapo maji yanawekwa dawa na kisha kupelekwa katika sehemu ya mtambo mwingine kwa ajili ya kusafishwa na kusafirishwa kwa wananchi.


(PICHA/HABARI NA MWANDISHI WETU)



Baada ya kazi ya kuunganisha umeme wa kutosha kukamilika 15 Aprili, 2017 kazi ya kuwasha pampu kubwa mpya za majighafi na majisafi katika Mtambo wa Ruvu Juu sasa imekamilika rasmi ambapo mtambo huo sasa umeanza kuzalisha lita milioni 196 kwa siku. Taarifa ya Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar Es salaam (DAWASA) inaeleza.


Ili kufikia uwezo huo wa uzalishaji kutoka lita milioni 82 zilizokuwa zikizalishwa hapo awali, kazi mbalimbali zilifanyika ikiwemo ujenzi wa kituo kipya cha kusukuma maji na ufungaji wa pampu mpya, maeneo mapya ya kusafisha maji, mitambo ya kuchuja maji, maeneo ya kuchuja tope na tenki kubwa la kuhifadhia maji safi.


Katika kuhakikisha kuwa maji hayo yanawafikia wananachi, kituo kipya cha kusukuma maji safi na salama kilijengwa sambamba na mabomba makuu ya kusafirishia maji hayo yenye jumla ya urefu  wa kilomita 70 kutoka Mlandizi hadi Dar es salaam.


Aidha, tenki jipya lenye uwezo wakuhifadhi lita milioni 10 limejengwa eneo la Kibamba lenye mwinuko; na kutoka hapo maji hushuka kwa nguvu ya mtiririko hadi katika matenki ya Kimara.


Kazi iliyokuwa imebaki ilikuwa ni kuongeza nguvu ya umeme ili kuwezesha pampu hizo mpya kufanya kazi. Hivi sasa kazi hiyo imekamilika, ukaguzi umefanyika na pampu moja baada ya nyingine zimewashwa ili kuhakiksha mfumo mzima sasa unafanya kazi.


Hadi kufika jana jioni (17 Aprili) maji yalikuwa yanaingia katika matenki yote kwa kupitia mabomba mapya bila matatizo. 


Mtambo huo wa maji wa Ruvu Juu sasa unapokea umeme wa kutosha kutoka katika transfoma kubwa iliyopo kituo kidogo cha umeme cha Chalinze (Sub-station) yenye uwezo wa 45/55 MVA ambapo inawezesha pampu zote mpya na za kisasa zilizofungwa kuwashwa kwa wakati mmoja.


Mikataba ya jumla ya dola za Marekani milioni 99 ya upanuzi wa mtambo na ujenzi wa mabomba mapya kutoka Ruvu Juu mpaka Kimara, ujenzi wa tanki kubwa lenye ujazo wa lita million 10, ofisi kwa ajili ya shughuli za uendeshaji wa huduma na nyumba za watumishi wa mtambo ilisainiwa mwaka 2014. Fedha hizo zilikuwa ni mkopo wa masharti nafuu toka Benki ya Exim ya India.


Kazi inayopewa msukumo mkubwa kwa sasa  ni ujenzi wa miundombinu ya usambazaji maji yaliyoongezeka ili wananchi wengi zaidi waweze kunufaika na jitihada na uwekezaji uliofanywa na Serikali yao.


Maeneo yanayonufaika ni pamoja na miji ya Kibaha, Mlandizi na baadhi ya Vitongoji vyake katika mkoa wa Pwani pamoja na maeneo yote yaliyopo jirani na barabara ya Morogoro yaani Kiluvya, Kibamba, Mbezi, Kimara, Ubungo, Malamba mawili, Msigani, Msakuzi, Makabe, Kibangu, External, Makuburi, Tabata, Segerea, Buguruni pamoja na Vingunguti.

MSANII WA BONGO FLEVA NILLAN AMPONDA SHILOLE

$
0
0


MSANII wa Bongofleva anayetamba na kibao cha ‘Njenje’ Gilbert Paul maarufu kama ’ Nillan' (pichani kulia) ameponda kitendo kilichofanywa na msanii  mkubwa katika  tasnia hiyo Zuwena Yusufu ‘Shilole’ cha  kuharibu Show iliyotarajiwa kufanyika mkesha wa siku ya mkesha wa Pasaka na hivyo kusababisha hasara kwa Promota.

Nillan aliyetarajiwa kufanya show siku pamoja na msanii mwingine Nuhu Mziwanda alisema kitendo kilichofanywa na Shilole siyo cha kiungwana kutokana na heshima kubwa aliyonayo msanii huyo kwa Taifa hili.

“Ukweli kitendo hicho mimi kama msanii chipukizi kimeniumiza sana, sikutaraji kingeweza kufanywa na msanii mkubwa na maarufu kama Shishi, namuheshimu kama dada yangu lakini kwa hili amejishushia heshima” alisema Nillan.

Show hiyo iliyokuwa imeandaliwa na Kampuni ya  Merry Merry Entertainment, ilishindwa kufanyika baada ya Shilole kuchelewa kufika ukumbini hali iliyosababaisha mashabiki waliofika mahali hapo kulalamika warudishiwe fedha zao na baadae kuondoka.

Akizungumzia baada ya tukio hilo Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Merry Mussa mbali na kulaani kitendo hicho cha Shilole alisema  ni lazima sharia itafuata mkondo wake kwa msanii huyo kulipa hasara yote iliyotokana na kitendo alichokifanya.

“Haiwezekani mtu tukubaliane afike  ukumbini saa  2 usiku, yeye anakuja  muda anaotaka, na hapo hapo hata kushuka kwenye gari hakushuka, hiyo ni dharau na kamwe sikubaliani na kitendo hicho hata kidogo” alisema Merry.

Shilole aliyetarajiwa kutoa burudani  siku hiyo ya mkesha wa Pasaka katika ukumbi wa Heinken uliopo Kijichi, aliwasili ukumbini hapo saa 7 za usiku tofauti na makubaliano na Promota aliyeandaa show hiyo.

Hata hivyo alipotafutwa Shilole kuzungumzia suala hilo alidai kufika ukumbini hapo kama taratibu zilivyo za wasanii kufika kwenye show mbalimbali hivyo haoni kama kuna kosa lolote alilifanya kuhusiana na show hiyo.
Kwa upande wake Nuhu Mziwanda aliyewah kuwa mahusiano na msanii huyo alikwenda mbali na kusema kitendo kilichofanywa na mpenzi wake huyo wa zamani ni ushamba na kumtaka kurudisha fedha alizochukua kutoka kwa promota.
Alisema anashangazwa kwanini Shilole alikubali kupokea fedha hizo na kuahidi kufanya show lakini badala yake akaingia mitini na kuibukia ukumbini muda ambayo show ilipaswa iwe mwishoni.


Akizungumzia suala hilo Meneja wa kampuni ya Ochu Entertainment  inayomsimamia msanii Nillan, Felix Mkuya alisema kitendo kilichofanywa na Shilole ni cha kushangaza na hakipaswi kufanywa na  wasanii wa hapa nchini.

“Imagine watu wametumia gharama kubwa kuandaa ile Show, kila msanii alishapewa hela yake mkononi, sasa kwanini yeye afanye vile, Nuhu Mziwanda alifika ukumbini mapema saa 12 jioni, alikadhalika kwa Nillan…sasa vipi Shilole afanye vile” alihoji Mkuya.

VIJANQ DAR WAANZISHA KLABU ZA KUPINGA MABADILIKO

$
0
0
Mwezeshaji wa Kisheria wa Shirika la Equality for Growth (EfG), Mariam Rashid (kulia), akitoa mafunzo ya kupinga ukatili wa kijinsia kwa vijana wafanyabiashara katika Soko la Ilala Mchikichini jijini Dar es Salaam kabla ya kufungua klabu za mabadiliko za kupinga ukatili huo katika soko hilo mwishoni mwa wiki.
Mwezeshaji wa kisheri Juliana Charles akichukua jina na maelezo kwa mfanyabiashara wa soko hilo aliyekubali kuwa mwana mabadiliko wa kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Mwezeshaji wa kisheria Charles Beatus (katikati), akiwa na vijana wa klabu ya wauza nguo za mitumba ya kike katika soko la Ilala Mchikichini wakibandika bango la mabadiliko.
Vijana wa mabadiliko wa Soko la Ilala Mchikichini wakiwa 
kataika picha ya pamoja.
Mwanasheria wa EfG, Muna Abdallah akichukua maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Klabu ya Mabadiliko ya wauza nguo za kike katika soko la Ilala Mchikichini, Adam Mohamed (kushoto)
wanamabadiliko wakionesha vipeperushi vya kampeni ya Tunaweza baada ya kufungua klabu hizo.
Mwezeshaji wa kisheria Zainabu Namajoji akichukua maelezo 
kwa wanamabadiliko.
Vijana wafanyabiashara katika Soko la Ilala Mchikichini jijini Dar es Salaam wakiwa katika picha ya pamoja na wawezeshaji wa kisheria wa Shirika la Equality for Growth (EfG), wenye fulana za njano, baada ya kufungua klabu ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia katika soko hilo mwishoni mwa wiki.

Maelezo yakichukuliwa.

Na Dotto Mwaibale

VIJANA wafanyabiashara katika masoko ya Temeke Sterio na Ilala Mchikichini jijini Dar es Salaam wameanzisha klabu za mabadiliko zitakazo saidia kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia masokoni kupitia kampeni ya miezi miwili ya Tunaweza inayofanywa na Shirika la Equality for Growth (EfG).

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na waandishi wa habari wafanyabiashara hao wamesema kwamba wameamua kuanzisha klabu hizo za mabadiliko na kushiriki kampeni hiyo baada ya kuhamasishwa na wasaidizi wa kisheria wa Shirika la Equality for Growth (EfG) kuhusu kutokomeza vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia katika maeneo yao ya biashara.

"Kampeni hii tumeikubali na ndio maana baada ya kuhamasishwa na EfG tumeamua kufungua klabu za wanamabadiliko kwani tumeona inatujengea mazingira mazuri ya kufanya biashara zetu katika eneo ambalo halina vitendo vya ukatili wa kijinsia" alisema Adam Mohamed ambaye ni Mwenyekiti wa klabu ya mabadiliko eno la wauza nguo za mitumba ya kike Soko la Ilala Mchikichini.

Alisema kwa muda mrefu katika soko hilo kulikuwa na kukithiri kwa vitendo hivyo lakini kupitia kampeni hizo imesaidia kuvipunguza na kuwa baada ya kupata mafunzo hayo kutoka EfG wamekuwa wakiifanya kampeni hiyo hata nje ya masoko ili jamii ijue umuhimu wa kuachana na vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia.

Mwenyekiti wa klabu ya wauza viatu na raba katika Soko la Ilala Mchikichini, Philip Chuwa alisema klabu zilizoanzishwa zitasaidia kukabiliana na vitendo hivyo kwa kuwa wanachama wake ni wafanyabiashara wenyewe hivyo itakuwa rahisi kumbaini mtuhumiwa na kumchukulia hatua.

Akizungumzia kampeni hiyo ya Tunaweza Mwanasheria na Mratibu kutoka Shirika la EfG, Mussa Mlawa alisema kampeni hiyo inaendeshwa na Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake Tanzania (WLAC) lakini katika masoko inafanywa na EfG.

Alisema lengo la kampeni hiyo ni kusukuma mabadiliko ya kupinga vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia masokoni na katika jamii.

Alisema kampeni hiyo kwa Dar es Salaam inafanyika katika masoko matano ya Ilala Boma, Mchikichini, Temeke Sterio, Buguruni na Ferry.

WANAWAKE KANISA LA PENTEKOSTE WAOMBA AMANI NCHINI ISUMISHWE

$
0
0
 Mwenyekiti wa Muungano wa Wanawake wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (MMPT) Misheni ya Kijitonyama,  Maines Mhama (kulia), akimkabidhi maua mgeni rasmi wa maadhimisho ya siku ya wanawake wa kanisa hilo, Anitha Mshighati (katikati), mara baada ya kuwasili kwenye sherehe hiyo iliyofanyika Kanisa la Pentekoste la Kituo cha Tabata Kisiwani Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Mchungaji Ibrahim Mshighati mume wa mgeni rasmi.


Hapa ni furaha tupu wakati mgeni rasmi akisindikizwa kuingia kanisani
 Mgeni rasmi Anitha Mshighati akizungumza katika maadhimisho hayo.
  Mwenyekiti wa Muungano wa Wanawake wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (MMPT) Misheni ya Kijitonyama,  Maines Mhama akizungumza kwenye maadhimisho hayo.
 Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Pentekoste Kituo cha Tabata Kisiwani, John Shusho akiwa kwenye maombi wakati wa maadhimisho hayo.
 Kwaya ya Kanisa hilo Kituo cha Tabata Kisiwani ikitumbuiza
 Nyimbo za kusifu zikiendelea.

 Kwaya ya Tabata Kisiwani ikiimba. 

Kwaya ya Kijitonyama ikiimba.
 Kwaya ya Gongo la Mboto ikifanya vitu vyake
 Kwaya ya Kipawa haikuwa nyuma kutoa burudani
 Mwimbaji wa nyimbo za injili wa kujitegemea, Joyce Agato akiwajibika
 Mwenyekiti wa Muungano wa Wanawake wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (MMPT) Misheni ya Kijitonyama,  Maines Mhama (kushoto), akiwa na wageni wake mgeni rasmi na mumewe.
 Ibada ikiendelea.
 Ni kuimba nyimbo za kusifu na kucheza.
 Mwenyekiti wa Wanawake Maines Mhama akitoa neno la maadhimisho hayo.
 Katibu Msaidizi wa Wanawake wa Kanisla hilo, Joyce Agato akimkabidhi risala mgeni rasmi.


Na Dotto Mwaibale

WANAWAKE  wametakiwa kuwa chachu ya kujenga  amani nchini badala ya kusubiri iharibike.

Mwito huo umetolewa Dar es Salaam mwishoni mwa wiki na Mwenyekiti wa Muungano wa Wanawake wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (MMPT) Misheni ya Kijitonyama,  Maines Mhama wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake kwa kanisa hilo.

"Wanawake tunapaswa kuwa wa kwanza kujenga amani ya nchi kuanzia kwenye familia zetu kwani inapokosekana waathirika wakubwa ni sisi na watoto wetu" alisema Mhama.

Alisema amani inapokoseka shughuli zote haziwezi kufanyika nchini ikiwa pamoja na kuabudu hivyo ni wajibu wa kila mmoja kuitunza kwani inapopotea gharama ya kuirudisha inakuwa kubwa.

Akiongelea matukio yanayotokea nchini ya watu kuuana kama yaliyotokea Kibiti mkoani Pwani kwa askari nane kuuana alisema wanadamu wanapaswa kumrudia mungu bila kujali itikadi za dini.

"Matukio ya kuuana yaliyoibuka hivi karibuni yatakwisha kwa watu kuwa na hofu ya mungu na si vinginevyo" alisema Mhama.

Mgeni rasmi kwenye sherehe hizo,  Anitha Mshighati aliwataka wanawake kuungana katika masuala mbalimbali na kuanzisha shughuli za ujasiriamali ili waweze kujikomboa kiuchumi.

"Wanawake serikali imetuwekea miundombinu mizuri ya kufanya shughuli zetu tutumie fursa hiyo kujianzishia miradi mbalimbali ili tuweze kufanya mambo makubwa ya kiuchumi" alisema  Mshighati.

Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni kuitafuta amani na kuidumisha.

NGORONGORO KITOVU CHA UTALII KINACHOWAVUTIA WATU MASHUHURI DUNIANI

$
0
0
Na Jumia Travel Tanzania

Inaonekana mwaka 2017 umeanza vizuri katika sekta ya utalii nchini Tanzania kutokana na watu kadhaa mashuhuri kuzuru vivutio vyake. Sehemu ambazo zimeonekana kuwavutia watu wengi zaidi ni hifadhi ya mbuga ya Serengeti na bonde la Ngorongoro.

Alianza mwigizaji maarufu wa filamu kutokea Hollywood nchini Marekani, Will Smith na mkewe Jada Pinkett-Smith. Mwanzoni mwa mwezi Machi walitua nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) na kujivinjari katika mbuga ya Serengeti. Wakiwa huko familia ya Smith walikutana na msanii mwingine kutokea huko huko Marekani, lakini huyu yeye ni mwanamitindo na mrembo, Chanel Iman.

Haikupita muda mrefu sana tangu watu hao mashuhuri kuwepo nchini, kwani siku chache zilizopita aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Taifa la Israel, Bw. Ehud Barak naye alitembelea mbuga ya Serengeti pamoja na Ngorongoro.

Hii ni ishara nzuri kwa sekta ya utalii nchini ambapo kupitia watu hawa maarufu wengine nao wanapata taarifa na kuhamasika kutembelea pia.

Lakini lazima tujiulize ni kwa nini Ngorongoro huwavutia watu zaidi na kuwafanya kufunga safari kuja Tanzania na sio sehemu zingine? Jumia Travel imekukusanyia vitu ambavyo vinapatikana katika eneo hilo la urithi wa dunia ambalo hakuna mtu atakayesimuliwa na kutotaka kulitembelea:

Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro. Kama ulikuwa haufahamu bonde la Ngorongoro ni shimo kubwa lililotokana na mlipuko wa volkeno ambalo halijai maji wala kubomoka duniani. Eneo hili ambalo limetangazwa kuwa ni urithi wa dunia na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO); lina urefu wa kilometa 20, kina cha mita 600 na ukubwa wa kilometa za mraba 300.

Vifuatavyo ni vivutio vinavyopatikana katika hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro:

Binadamu na Wanyama kuishi pamoja. Kwa zaidi ya miaka 200 iliyopita watu wa kabila la Wamasai walifika eneo hili na kuishi hapo. Maisha yao ya jadi yamewafanya waweze kuishi pamoja na mifugo yao kwa amani na utulivu kabisa bila ya kuwabugudhi wanyamapori. Mpaka hivi sasa kuna wafugaji wa Kimasai takribani 42,000 wakiishi katika hifadhi pamoja na mifugo yao kama vile ng’ombe, punda, mbuzi na kondoo. Kipindi cha mvua hutoka eneo hili na kuelekea maeneo ya tambarare ambapo kiangazi kikifika hujisogeza maeneo ya karibu ya mlima na misitu iliyopo. Wamasai huruhusiwa kuingiza mifugo yao kwa ajili ya kuilisha na kuinywesha lakini si kufanya shughuli za kilimo; lakini maeneo mengine ya hifadhi wanaruhusiwa kurandaranda.

Bonde la Volkeno na Wanyamapori. Bonde la Ngorongoro lilitokana na mlipuko wa volkeno takribani miaka milioni 3 iliyopita ambapo ni kubwa, lisilobomoka wala kutojaa maji. Lilitangazwa na UNESCO kuwa ni urithi wa dunia mwaka 1979 na ni eneo pekee ambalo binadamu, mifugo na wanyama wanaishi kwa pamoja kwa amani na utulivu kabisa. Unaweza kukuta kuna wakati ng’ombe wa Wamasai wanachunga pamoja na pundamilia katika mbuga za Ngorongoro.      

Masalia ya Kale ya Binadamu wa Mwanzo. Ngorongoro ndimo linapopatikana bonde la Olduvai ambalo kwa mujibu wa wanahistoria yanapatikana masalia ya binadamu wa mwanzo kuishi duniani. Hapa ndipo wanaikolojia maarufu Dkt. Louis na mkewe Mary Leakey walipata masalia ya kale likiwemo fuvu la mtu wa kale zaidi, Zinjanthropus, ambaye alipata kuishi miaka milioni 1.75 iliyopita. Utafiti wao uliweza kuvumbua mabadiliko ya taratibu ya ukubwa wa ubongo na zana zao za mawe walizokuwa wanazitumia.

Vivutio vingine. Mbali na vivutio vilivotajwa hapo juu pia kuna vitu vingine chungu nzima vya kuvutia watu wanavyoweza kuvifurahia kuviona.

Ziwa Ndutu na Masek; maziwa haya hujaa kutokana na maji yanayotiririka kutokea milimani, na maji yake hayafai kwa matumizi ya binadamu kutokana na chumvi nyingi iliyonayo.



Oldonyo Lengai; hili ni jina la lugha ya Kimasai likiwa na maana ya ‘Mlima wa Mungu,’ unapatikana nje kidogo ya hifadhi ya Ngorongoro. Ni mlima pekee wenye volkeno hai ambapo ilishawahi kulipuka mwaka 2006 na siku za hivi karibuni mwezi Julai mwaka 2007.

Mchanga Unaohama; safu ya mchanga mweusi umetakana na majivu ya mlima wa volkeno wa Oldonyo Lengai, umekuwa ukisukumwa taratibu kuelekea upande wa Magharibi wa hifadhi kwa kiwango cha mita 17 kwa mwaka. Una kimo cha mita 9 na mzingo wenye urefu wa mita 100, unapatikana Kaskazini mwa bonde la Olduvai.  




Bonde la Olkarien; eneo hili nalo ni muhimu katika hifadhi kwani hutoa hifadhi kwa ndege tai aina ya Ruppell Griffon. Msimu mzuri wa kutembelea eneo hili ni miezi ya Machi mpaka Aprili ambapo tai huzaliana. Wanyama huja eneo hili pale panapokuwa na malisho ya kutosha.


Kutazama ndege aina ya Flamingo na wengineo wa kila aina. Ndege aina ya Flamingo wanaonekana sana katika maziwa yanayopatikana ndani ya hifadhi. Mbali na ndege hao pia kuna aina mbalimbali za ndege ambao wanaweza kuonekana katika misimu tofauti ya majira ya mwaka hususani miezi ya mvua.

Safari ya Kuizunguka Hifadhi. Utakuwa hujaifaidi Ngorongoro kama haujavizungukia vivutio mbalimbali vinavyopatikana ndani yake. Kwa kuwatumia waongozaji wa mbuga, hakikisha kwamba unatembelea sehemu kama vile bonde la Olmoti kuelekea nyanda za Embakai, shuka chini kuelekea Bonde la Ufa, pandisha Kaskazini kwenye nyanda za hifadhi ya misitu na kisha eneo la tambarare la Mashariki kuzunga miamba ya Nassera, milima ya Goli na bonde la Olkarien.  

Kwa hakika hii ni Edeni ya sasa kama watu wengi wanavyopenda kuiita kutokana na maajabu iliyonayo pamoja na historia ya binadamu wa mwanzo kuishi mule. Sasa kama watu wanasafiri kutoka kila pembe ya dunia kuja kulitembelea eneo hili kwa nini na wewe mtanzania usitenge muda na kupanga kufanya hivyo? Haihitaji kuwa milionea kutembelea eneo hili, kunafikika kwa urahisi na hata malazi ni nafuu pia kwani Jumia Travel wamekurahisishia hilo.

NHIF YABORESHA HUDUMA ZAKE

Viewing all 1941 articles
Browse latest View live