Quantcast
Channel: BONGOWEEKEND
Viewing all articles
Browse latest Browse all 1909

ALHAJI MANSOOR ATOA SADAKA YA RAMADHAN KONGOWE MKOANI PWANI

$
0
0



Alhaji Mussa Mansoor  amesema kwamba amekuzwa katika utaratibu wa kusoma Dua ya kurehemu baba yake Mzazi ,Viongozi mbalimbali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao wametamgulia mbele ya haki.

"Jambo hili  la kusoma Dua na kutoa sadaka nalifanya kwa zaidi ya miaka 12 sasa"amesema Alhaji Mansoor. 
Mansoor  amesema hayo leo Februari 28 wakati alipozungumza  na Waandishi  wa Habari mara baada ya kumaliza kusoma Dua iliyofanyika nyumbani kwake Kongowe Kibaha  Mkoani Pwani.

"Huwa natoa sadaka ya futuri kwa  waumini wa dini zote huku nikielewa kwamba Ramadhani  ya kwanza huwa inakuwa  ngumu hivyo nimetoa sadaka ya futari ambayo ni kianzio kwa mwezi mtukufu  nimetoa sadaka  ya futari kwa watu wa imani zote ilimradi amefika hapa basi kila mmoja anapata  mzigo wake" amesema Alhaji Mansoor. 

Amesema kuwa kwenye Quran tumeusiwa sana suala la kutoa sadaka  pia  waalimu wetu wanasema kuwa  siku nzito kwa mwanaadamu ni siku yake ya kwanza kaburini ambapo mtu huomba kwa Allah arudishwe duniani ili aweze kutoa sadaka  hivyo basi wote tudumu kwenye kutoa sadaka hivyo basi Inshaallah  Mwenyeezi Mungu atujaalie tuufunge mwezi mtukufu wa Ramadhani  salama na tumalize salama,amesema Alhaji Mansoor.
Mhe.Mansoor akiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kusoma Dua na baadhi ya Masheikh waliosoma Dua ya kurehemu Viongozi,  baba mzazi  wa Mansoor pamoja na waislamu wengine  waliotangulia mbele ya haki ikiwa ni utaratibu  wake katika kuupokea Mwezi  Mtukufu wa Ramadhani. 

Viewing all articles
Browse latest Browse all 1909

Trending Articles