Quantcast
Channel: BONGOWEEKEND
Viewing all articles
Browse latest Browse all 1915

WAUGUZI KATOENI HUDUMA KWA KUMTANGULIZA MUNGU -KIMITI

$
0
0

 













ALIYEKUWA Kada wa Chama na kiongozi aliyeshika nyadhifa mbalimbali  Serikalini Mbunge Mstaafu  Sumbawanga Paul  Petro Kimiti amewataka Wauguzi kote nchini kutoa huduma hiyo kwa wahitaji kwa kumtanguliza Mungu sababu kazi yao inahitaji Imani zaidi.

Kimiti amesema  hayo kwenye maadhimisho ya siku ya Wauguzi Duniani ambayo imeadhimishwa  Kimkoa Mkoa wa Pwani    hivi karibuni 
 huku akiwasisitiza  watoe huduma kwa kuzingatia hofu ya Mungu zaidi ikifuatiwa na maslahi yao.

"Huduma yenu mnaoitoa kwa wagonjwa ni ya kiimani na mnapaswa kuelewa kwamba mfahamu kuwa  hii ni ibada na malipo yenu yako kwa mungu " amesema Kimiti.

Aidha amewataka Maofisa Utumishi kushughulikia madai kwa watumishi ambao bado hawajalipwa stahiki zao ili kuwajenga mioyo wauguzi hao  waweze kutoa huduma  kwa wito kwa wagonjwa Hospitalini.
 
Kimiti amewapongeza wauguzi wa Mkoa wa Pwani kwa kazi kubwa wanayofanya na  kwamba Serikali inatambua changamoto wanazopitia ndiyo maana kwasasa nguvu kubwa imeelekezwa katika kuwasaidia Wauguzi ili  waweze kupata haki zao za msingi.
 
Aidha Chama Cha Wauguzi (TANA) kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya Chalinze wanatarajia kujenga chuo cha Uuguzi na Ukunga kwa kutumia majengo ya ofisi za awali za Halmashauri hiyo ambapo wameomba kusaidiwa kupata wadau wa kufanya ukarabati na ununuzi wa vifaa ili waweze kukamilisha hatua za kuanzisha chuo hicho.
Katika maadhimisho  hayo Wauguzi walikula  kiapo Chao huku wakiwasha mishumaa.

" Wauguzi mnaapa kila mwaka kwa ajili kukumbushwa wajibu wenu hivyo mkafanye kazi  kwa maadili na kuheshimu kiapo chenu" amesema Mganga  Mkuu wa Mkoa wa Pwani Dkt.Kusilie Ukiyo.
"Wauguzi tujiulize  kwanini tunaapa kila mwaka katika taaluma zingine huwa hawaapi kila mwaka  kama ninyi hivyo endeleeni  kukiishi kiapo chenu timizeni wajibu wenu mbele ya Mwenyeezi Mungu " amesema Dkt. Ukio.

 Aidha Dkt. Ukio ameahidi  kuboresha maadhimisho ya wauguzi katika siku zijazo.

"Dkt.Ukui amesema kuwa  ndani ya miaka mitatu kiasi cha Bil.25 zimetumika katika sekta ya afya Mkoa wa Pwani,pia naahidi kuwa  tutalifanyia kazi suala la upungufu wa wafanyakazi vifaa tiba  na tunawapongeza kwa kufanya kazi  bika kukata tamaa na serikali  inatambua na kuthamini huduma na kazi yenu kwani bila uuguzi hakuna huduma  bora kwa mgonjwa" amesema Dkt. Ukui.

Wakati huohuo Dkt.Ukui amekemea tabia ya wananchi kujichukulia sheria  mikononi mwao kwa kuwapa vipigo wauguzi amesema kuanzia sasa sheria itachukua mkondo wake.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Wauguzi  amewapongeza Wauguzi hao kutokana na huduma wanayoitoa kwa kusema kuwa  Wauguzi wengi ndiyo wanaoongoza katika Zahanati nyingi nchini,"ninyi mnafanya kazi kubwa  nchini  msichoke  changamoto  zenu za malipo ya kazi za  ziada  katika kila kituo tutaweka miongozo mizuri" amesema.

Wauguzi hao wametakiwa kupunguza  vifo vya mama na mtoto huku akisisitiza  wauguzi hao na kusema kuwa   huduma za Uuguzi  na Ukunga  zinasimamiwe  na maadili  bora ya kitaaluma.

"Mgonjwa  au mteja  anapofika Kituoni au Hospitali  anatajia  kupata  maneno  ya upendo na faraja zingatieni hilo.



Viewing all articles
Browse latest Browse all 1915

Trending Articles